Tuesday, December 23, 2008
Maisha ni wengine kupata tabu na wengine kupata rahaa

Hapa Jerry wa ITV akimuoji mtoto aliyekutwa amekatwa katwa katika mwili wake na watu tusiowajua
Kama kawaida yetu tunajazana kibao kila mtu anataka yeye aone kwanza

Hiki sio kiota cha ndege bali ni nyumba ya huyo mtoto aliyojenga juu ya mti! Bwana maisha hayaaaaa
Hapa watu wenye imani walimfunika huyo mtoto .Tukio lenyewe limetokea leo maeneo ya bonde la mkwajuni K-ndoni
Inasemekana Mtoto alipigwa huko Mwananyamala na watu tusiowajua na kumkatakata mwili wake
Baadaye huyo mtoto akajikongoja mpaka kwenye maskani yake yalio juu ya mtii. Alipozidiwa akashuka na kulala
njiani, ndipo watu walipoanza kujazana na ukiona wenzako wanashangaa nawe utataka kushangaa pia ndipo nami nikataka kujua kulikonii
Picha zote Nokia N80
Posted by Unknown at 12/23/2008 01:19:00 PM
Monday, December 22, 2008
Dawasco yapigwa mwereka bei ya maji
Rufaa ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (Dawasa) ya kutaka iruhusiwe kupandisha gharama za utoaji wa huduma ya majisafi na
Rufaa ya Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (Dawasa) ya kutaka iruhusiwe kupandisha gharama za utoaji wa huduma ya majisafi na
Posted by Unknown at 12/22/2008 10:59:00 AM
'Dudu' Kagoda lilivyonyakua mabilioni BOT:: Soko la Kariakoo hoi
Posted by Unknown at 12/22/2008 10:40:00 AM
Sunday, December 21, 2008
KWA TULIOSOMA OYSTERBAY PRIMARY SCHOOL
Jamani wale wote tuliosoma shule ya msingi Karume au Oysrerbay Primary School
Toka enzi za Ukoli mpaka leo hii. Tunatakiwa tukajiunge na Oysterbay
Primary School Group kwa kutuma ujumbe wa barua pepe kwenda Link hii Oysterbayprimary-subscribe@yahoogroups.com ili ujiunge na Group
Katika group hiyo ina mipango ya kusaidia shule yetu pia kupanga reunon
Group hii imeanzishwa na watu waliosoma kati ya miaka ya 1980 na wale wote tuliosoma hapo
Kama una dukuduku lolote usisite kuuliza kupitia link hii Oysterbayprimary-subscribe@yahoogroups.com Mnakarishwa wote
Wenu John="
Posted by Unknown at 12/21/2008 06:47:00 PM
Saturday, December 20, 2008
Subscribe to:
Posts (Atom)















