Friday, February 24, 2012
Thursday, February 23, 2012
WATU wawili wafariki mkoani Pwani
Na John Gagarini, Kibaha
WATU wawili wamekufa mkoani Pwani kwenye matukio mawili tofauti
likiwemo la wananchi wenye hasira kali kumwua kwa kumpiga Bw Idrisa
Ugandi (26) mkulima na mkazi wa Kiomboni Visiwani Wilayani Rufiji
baada ya kumtuhumu kuvunja na kuiba vitu mbalimbali vyenye thamani ya
shilingi 935,000.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana mjini
Kibaha na kamanda wa polisi mkoa wa Pwani Bw Ernest Mangu alisema kuwa
marehemu alikuwa na wenzake wanne ambao walikimbia kusikojulikana.
Kamanda Mangu alisema kuwa tukio hilo lilitokea Februari 21 mwaka huu
majira ya saa 5:00 asubuhi huko Kijiji cha Mlanzi wilayani Rufiji.
Akielezea juu ya tukio hilo alisema kuwa marehemu na wenzake walivunja
nyumba ya Bw Salum Hija akiwa na wenzake na kufanikiwa kuiba vitu
mbalimbali ikiwa ni pamoja na fedha taslimu sh 800,00, simu mbili za
mkononi zenye thamani ya sh 80,000, redio ndogo yenye thamani ya sh
25,000, suruali moja aina ya Jeans sh 15,000, kanga doti moja sh 8,000
na kitenge doti moja 7,000.
Alisema kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa kwenye kituo cha afya
Mlanzi kusubiri uchunguzi wa daktari na ndugu wa marehemu kwa mazishi
pia hakuna mtu aliyekamatwa kuhusinana na tukio hilo na polisi
wanaendelea na uchunguzi.
Wakati huo huo mtoto Makia Karimu mwenye umri wa miaka (6) Mkazi wa
Bungu wilayani Rufiji amekufa baada ya kugongwa na pikipiki wakati
akitembea kwa miguu.
Kamanda Mangu alisema kuwa tukio hilo lilitokea Kiiji cha Bungu majira
ya saa 1:30 usiku barabara kuu ya Dar es Salaam Kilwa ambapo aligongwa
na mwendesha pikipiki aliyetambuliwa kwa jina la Raphael aliyekimbia
akiendesha pikipiki yenye namba za usajili T 419 aina ya Sanlg, chanzo
cha ajali hiyo ni mwendo wa kasi.
mwisho.
Posted by Kennedytz at 2/23/2012 04:52:00 PM
Capital News--World Bank report-Road infrastructure development--Moshi rain--Road sefety--
World Bank report-Road infrastructure development--Moshi rain--Road sefety--
Posted by Unknown at 2/23/2012 04:15:00 PM
Wednesday, February 22, 2012
Msukosuko wa uchumi na matatizo yanayojitokeza
Tanzania yatakiwa kubana matumizi ya serikali ili kuepuka uchumi kuyumba
Posted by Unknown at 2/22/2012 08:33:00 PM
Mgomo wa madereva wa Hiace Kilimanjaro- Meli ya iliyokatwa na samaki ya...
Posted by Unknown at 2/22/2012 08:26:00 PM
Capital TV na habari za Tanzania
Development vision 2015 and Climate change reseach. Tampered fuel pumping machine
Posted by Unknown at 2/22/2012 12:04:00 AM
Tuesday, February 21, 2012
Monday, February 20, 2012
Saturday, February 18, 2012
Friday, February 17, 2012
Habari za Tanzania via Kennedytz
Leo pata habari toka TBC
Posted by Unknown at 2/17/2012 01:05:00 PM
Thursday, February 16, 2012
Monday, February 13, 2012
Habari za Tanzania via Kennedytz
Askari wa wanyama pori wanyanyasa wafugaji. Chadema yaendelea kutoa somo katika katiba elekezi ya Tanzania. Waislam nao wajianda kutoa masomo katika katiba elekezi ya Tanzania.
Posted by Unknown at 2/13/2012 11:24:00 AM
Vichaka katika mji wa kigamboni ni kero kwa raia
Jeshi la polisi latakiwa kuwa makini na vichaka Kigamboni. Serikali na changamoto ya kujivua gamba. Halmashauri kuu ya CCM yakutana Dodoma.
Posted by Unknown at 2/13/2012 10:39:00 AM
Thursday, February 9, 2012
Sakata la mgomo wa madokta lapelekea waziri na katibu mkuu wake kusimami...
Maendeleo ya Mgomo wa madaktari nchini Tanzania yamesababisha waziri wa wizara ya afya na katibu wake kusimamishwa na jeshi la polisi kuchunguza kulikoni'
Kuanzia kesho madaktari wote watakiwa kuanza kazi mara moja ili kupunguza giza nene kwa wagonjwa katika hospitali mbalimbali ndani ya Tanzania.
Posted by Unknown at 2/09/2012 09:19:00 PM






