Friday, December 21, 2007





Father Christmas akimkabidhi zawadi ya T-shirt na juisi mshindi Toka

cocacola .

Posted by Picasa

Thursday, December 20, 2007

ni mwaka mmoja wa HabariLeo


::Maskani>habari
Habari za KitaifaHabari nyingine zaidi!
Ni mwaka mmoja wa HabariLeo
Mwandishi Wetu
HabariLeo; Thursday,December 20, 2007 @00:03
GAZETI pekee la serikali la Kiswahili la HabariLeo linalochapishwa na Kampuni ya Tanzania Standard Newspapers (TSN), kesho linatimiza mwaka mmoja tangu lilipoanzishwa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Meneja Masoko wa TSN, Christina Geleja, kwa niaba ya Mhariri Mtendaji, sherehe hizo zitafanyika katika jengo la TSN Mtaa wa Samora, Dar es Salaam, kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa sita mchana.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo anatarajiwa kuwa Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi.

Alisema sherehe hizo zitaambatana na maelezo kuhusu maendeleo ya Kampuni na mafanikio ya gazeti hilo, kuzindua shindano la wasomaji wa HabariLeo, utoaji wa zawadi kwa wauzaji bora wa HabariLeo, hotuba ya mgeni rasmi na burudani maalumu.

Gazeti la HabariLeo lilianzishwa Desemba 21, 2006, ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2005 hadi 2010, ambayo katika eneo la vyombo vya habari, pamoja na mambo mengine, iliahidi kuanzisha gazeti la Kiswahili la Serikali.

Rais Jakaya Kikwete ndiye aliyezindua gazeti hilo kwenye Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma, asubuhi ya Desemba 21, 2006, ikiwa ni mwaka mmoja tangu atawazwe kuwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne ya Tanzania.

Mbali ya kumiliki gazeti hilo, TSN pia inamiliki magazeti ya Kiingereza ya Daily News na Sunday News, ambayo ni magazeti yanayoaminika nchini katika lugha ya Kiingereza. Pia ndiyo magazeti kongwe nchini.

Kutokana na shughuli hiyo, Mtaa wa Samora kuanzia makutano ya Mtaa wa Mkwepu na hadi makutano ya Barabara ya Azikiwe, utafungwa kwa muda kupisha shughuli hiyo.
Copyright @TSN 2006 All Rights Reserved
Posted by Picasa

Wednesday, December 19, 2007

EA awaits historic Kenyan election





EA awaits historic Kenyan election

THE EAST AFRICAN COUNTRIES ARE WATCHing the Kenyan general election very keenly, as it is expected to have a major impact on the growth of democracy in the region.

Particularly under scrutiny is the Electoral Commission of Kenya (ECK), which has grown to be one of the most important institution of governance in East Africa.

Apparently, election management — from the transportation of ballot papers and the actual voting to the tallying of results — is still a nightmare in most African countries. Indeed, some of the electoral bodies who refer to themselves as “independent” have often presided over palpably flawed elections, as in the recent case of Nigeria.

The Kenyan electoral body for its part has come a long way from the time when its members were appointed by the all-powerful president to serve his whims, to the 1997 inter-party minimum electoral reforms that allowed various parties to nominate commissioners to the electoral body.

Notably, the ECK has moved from being perceived as a tool of the executive to an independent entity that enjoys the confidence of over 50 per cent of Kenyans.

More encouraging is that unlike other public institutions such as the Kenya Anti-Corruption Commission and the Kenya National Commission on Human Rights that gobble up huge public resources, the ECK has managed to use its resources to increase its capacity in terms of logistics and investment in technology.

By coming out to admit that some constituencies may not hold parliamentary and civic elections due to a mix-up in ballot papers — a contingency he later clarified was unlikely — ECK chairman Samuel Kivuitu, has demonstrated that he is willing to keep Kenyans informed as far as emerging hitches are concerned.

The challenge for the ECK is to correct the mistakes in time and in a manner that instils confidence in the affected constituencies. Ironically, Kenya has not witnessed the extent of mix-up the ECK is talking about in the past two elections, when the body enjoyed less confidence among Kenyans.

The 2007 poll is perhaps the most critical election in Kenya’s independent history, since the number of parliamentary seats garnered by political parties will determine whether Kenyan will be governed by one party or a coalition government.

MR KIVUITU FOR HIS PART HAS TO PROVE that the honour bestowed on him last week by the International Commission of Jurists for his independent mind and the gall to stand up against political pressure, was not in vain.

But as other regional countries look to Kenya to lead the way by holding free and fair elections, the biggest challenge in East Africa is how to practise democracy in between elections. It has been a general assumption that holding elections on schedule is enough to prove a country’s democratic credentials, while governments in the region continue with undemocratic practices in between elections.

These include official corruption, lack of accountability, incapacitation of watchdog institutions and the harassment of the media. It is not unknown for governments in the region to shut down television stations, raid media houses, intimidate journalists, while at the same time priding themselves on the fact that they hold periodic elections.

All the same, ECK has won admiration in the region for holding a satisfactory

Posted by Picasa




Cartoon by GADO: [Published on Monday, November 27, 2006]
Posted by Picasa




Posted by Picasa




Posted by Picasa

Tuesday, December 18, 2007

Jacob Zuma is the new ANC leader


Jacob Zuma is the new ANC leader

New ANC leader Jacob Zuma

Jacob Zuma has been elected as the new leader of the ANC

December 18, 2007, 21:15

Jacob Zuma is the new President of the ANC. Zuma secured 2 329 votes. He was up against incumbent President Thabo Mbeki for the party's top position. Mbeki received 1 505 votes. Zuma also emerged as the frontrunner during the party's recent nomination process.

He secured nominations in five provinces, including Gauteng, KwaZulu-Natal, Mpumalanga, the Free State and the Northern Cape. The ANC Youth League and Women's League also stood firmly behind him. Mbeki garnered votes from the ANC in the Eastern and Western Capes, the North West and Limpopo.

Dren Nupen, the head of the Elections Agency tasked with overseeing the election process, made the announcement.

Former Secretary General Kgalema Motlanthe has been as the new Deputy President for the ANC. He was pitted against Foreign Affairs Minister Nkosazana Dlamini-Zuma.

National Speaker of Parliament Baleka Mbete has defeated Government's Policy Co-ordinator, Joel Netshitenzhe, to the position of National Chairperson.

The SA Communist Party (SACP) Secretary General Gwede Mantashe won the race for the party's National Chairperson. The other contender was the National Chair, Mosiuoa Lekota.

Speaker of the North West Legislature, Thandi Modise, is the new Deputy Secretary General. She was up against Public Works Minister, Thoko Didiza. Matthews Phosa is the new Treasurer-General of the party.

Posted by Picasa

Tatizo kocha anachonga sana Kisa kaletwa na .........

Posted by Picasa



Michezo
Kombe la Chalenji layeyuka
Emmanuel Mrema
HabariLeo; Tuesday,December 18, 2007
Mshambuliaji wa timu ya Kilimanjaro Stars Erasto Nyoni (mbele) pamoja na mlinzi wa pembeni Ziriab Hussein wa Sudan wakiwa chini baada katika harakati za kugombea mpira wakati wa mchezo wa pili wa robo fainali baina ya timu hizo mbili uliochezwa jana katika uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam. Sudan ilishinda 2-1.(Picha na Mroki Mroki)
MATUMAINI ya Tanzania Bara kunyakua Kombe la Soka la Chalenji baada ya takriban miaka 13, yaliyeyuka jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam baada ya kucharazwa mabao 2-1 na Sudan katika mechi ya robo fainali ya michuano hiyo ya Afrika Mashariki na Kati.

Ikicheza mbele ya mashabiki waliojazana kwenye uwanja huo, Tanzania Bara ‘Kilimanjaro Stars’ haikuonyesha kiwango kizuri katika kipindi cha kwanza, hali iliyowaruhusu wachezaji wa Sudan kutawala mchezo huo watakavyo.

Baada ya mechi hiyo, wachezaji wa Kili Stars wakiwa wameinamisha vichwa vyao chini walikimbia kwenye vyumba vyao ili kuepuka mashabiki wenye hasira kuwadhuru.

Kwa muda wote wa mechi hiyo, mashabiki wa soka waliokaa jukwaa kuu katika upande unaotumiwa na mashabiki wa Simba walionekana kuishangilia Sudan kwa nguvu huku wakiimba nyimbo za shangwe.

Sudan, timu pekee kutoka Afrika Mashariki na Kati, iliyofuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika zilizopangwa kufanyika mjini Accra, Ghana, Januari mwakani, ilianza kuhesabu bao la kwanza katika dakika ya 10.

Bao hilo lilifungwa na Abdelhamid Amarria kwa ufundi akiwaacha wachezaji wa Kili Stars wasijue la kufanya.

Dakika 15 baadaye, Daniel Mrwanda anayecheza soka ya kulipwa Kuwait aliisawazishia Kili Stars bao hilo baada ya kuunganisha mpira wa kona na kuujaza wavuni.

Ikiwa bado inatafakari jinsi ya kuongeza bao la pili, Kili Stars ilijikuta ikipachikwa bao jingine, mfungaji akiwa yuleyule Amarria.

Kili Stars ilibadilika kipindi cha pili na kufanya mashambulizi ya hapa na pale katika lango la wapinzani wao na kama Nizar Khalfani angekuwa makini angeweza kuisawazishia timu yake bao dakika ya 85 kwa mkwaju wa penalti.

Khalfani anayecheza soka ya kulipwa Kuwait alipiga penalti hiyo, lakini alikosa baada ya mkwaju wake kupanguliwa na kipa wa Sudan, Mohamed Adam.

Penalti hiyo ilitolewa na mwamuzi wa mchezo huo, Ally Kalyango wa Uganda baada ya mchezaji Vincent Barnabas kuchezewa vibaya eneo la hatari.

Akizungumza baada ya mechi, Kocha wa Kili Stars, Marcio Maximo, alisema bahati haikuwa yao kwani timu yake ilicheza vizuri hasa katika kipindi cha pili.

“Hakuna wa kumlaumu, timu nzima ilicheza na imepoteza ushindi… hiyo ni changamoto kwa wachezaji na kwa sasa najipanga kujiandaa na mechi za awali kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia mwaka 2010,” alisema raia huyo wa Brazil.

Katika mechi nyingine ya robo fainali iliyochezwa jana, Burundi iliifunga Eritrea mabao 2-1.

Mabao ya Burundi yalifungwa na Claude Nahimana dakika ya 68 na Aime Nzohabonayo dakika ya 80 na lile la Eritrea lilifungwa na Berhane Aregaye dakika ya pili.

Kilimanjaro Stars: Ally Mustapha, Salum Sued, Erasto Nyoni, Meshack Abel, Shaaban Nditi, Mrwanda, Castory Mumbara, Michael Chuma, Uhuru Selemani, Nizar na Amiri Maftaha.


Sudan: Mohamed Adam, Ziriab Hussein, Ahmed Elbasha, Abdelhamid Amarria, Balla Gabir, Saifeldin Ali Idrisa, Nasredin Omer, Adir Bokhari Omer, Modather Eltaab, Anas Eltaher, Khalid Hassan, Akram Elhadi Salim.
Copyright @TSN 2006 All Rights Reserved
Posted by Picasa

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.comme google-site-verification=Qm-XNfnL5kai8WV2inT1RRX2WIPaBTG_WPq3kYSBwbgKennedy Kimaro 2008 NYUMBANI NI NYUMBANI TU KUMBUKA KUWEKEZA NYUMBANI LEO

Rudi TOP-Juu