Saturday, September 21, 2019

SIMULIZI YA MZUNGUKO WA MAISHA YETU YA KILA SIKU

Leo tarehe 21 sept 2019 Jumamosi ilikuwa siku ya kawaida kwangu Kama jumamosi nyingine.

Niliamka muda ambao uwa ni kawaida yangu siku zote.

Nilichukua mswaki nikaweka dawa ya mswaki ninyotomia kila siku aina ya whitening.

Uwa natoka nje ili nijifanyie mazoezi kidogo kupasha mwili moto na kuweka viungo sawa.

Niliondoka nyumbani saa mbili na dakika kadhaa nikawa nipo nje ya muda ambao sio rafiki

Nilipofika maeneo ya jirani na kazini nilienda kutafuta chapati moja ili niweke na ndizi nilizowekea na mke wangu kipenzi.

Kulikuwa hakuna chapati kisa anayezikaanga mkaa ulikuwa aujakolea moto..

Nikawasha gari kuelekea kazini.

Pembeni kulikuwa na vibanda vya mama lishe zaidi ya kimoja.

Katika kibanda kimojawapo walikuwepo wafanyakazi wenzangu wawili.

Ilinibidi nipaki gari  karibu na walipopaki gari lao.

Nilipofika tukasalimiana nao uku nikivuta kiti na kukaa.

Wao walikuwa wakisubiri kifungua kinywa walicho kiagiza asubuhi hiyo.

Nikajeuka upande waliopo mama rishe na kuwauliza mtori upo.

Nilijibiwa na mmoja wao upo tele.

Nikawaambia lazima niuonje kwanza kabla ya kunywa.

Wakati nasubiria ili niuone uo mtori

Kumbe wenzangu nao walikuwa wanasubiri mtori pia.

Ukaletwa mtori wao bakuli mbili na chapati moja kwa kila bakuli.

Nami nikasema nipewe  mtori kama ulioletwa kwa wenzangu.

Wakati bakuli yangu yenye mtori na chapati inafika mezani,

Kwa mbali Mzee mmoja alikuwa anakuja upande wetu akiwa mnyonge na upole kidogo.

Nikanyanyua kijiko na kuonja ule mtori kama unafikia kiwango cha kufanana na mtori.

Nilipouonja testi yake ilikuwa mtori ni mwepesi sana wakati kawaida ya mtori ndizi zinakuwa nyingi kuliko maji.

Nikauliza ni shilingi ngapi bakuli moja na chapati moja.

Kwa mbali mama lishe akanijibu ni elfu moja na mia mbili hivi.

Wakati huo yule babu alikuwa amefika karibu yetu

Nilipomuona tu na onyonge wake, basi kama kawaida yangu huruma umetawala fikra zangu

Mungu akaniambia msaidie huyo mzee hili asubuhi iwe ya furaha kwake pia.

Bila kusita nikajeuka kwa  yule mzee na kumwambia karibu upate mtori huku unikitumia jina babu.

Yule Mzee  akacheka kwanza na kusimama pale alipo kwa sekunde chache.

Mzee akajeuka upande wetu na kuelekea katika  meza iliyo karibu yake.

Alivuta kiti na kukaa kusubiria aletewe mtori na mama lishe.

Ndipo nilpowajeukia mama lishe na kuwasisitiza walete mtori kwa Mzee.

Najua unashangaa kuona natoa hisani ya mtori kwa huyo mzee na nimepata wapi nguvu kama hiyo.

Nguvu ya Upendo kwa binadamu kusaidiana wenyewe kwa wenyewe  inatokana na upendo wa Yesu kwetu.

Yesu litenda maajabu na kutufundisha mengi yenye hekima ili iwe mifano na mafunzo kwetu daima milele.

Katika safari zake nyakati hizo watu walikuwa wakimfuata ili wasikilize mafundisho yake.

Ndipo siku moja walipokusanyika watu wengi na kukosekana chakula cha kuwapa

Ndipo

Yesu alichukua vipande mikate na Samaki ili wote waliofika katika mkusanyiko wapate chakula.

Nguvu ya kuwalisha umati wa watu alionyesha Yesu ni nguvu ya Mungu baba kwetu ili sisi kupata msamaha wa dhambi zetu.

Nikatoa noti ya elfu kumi na kumpa mama lishe.

Ili iwe malipo ya mtori kwa sisi watatu na yule babu.

Mama lishe akanipa chenji yangu  nami nikaipokea na kuiweka mfukoni tayari kwa kuondoka eneo hilo.

Sisi tulielekea kazini kama kawaida yetu Ila muda huo tukawa tumechelewa kidogo.

Tulianza kazi kama kawaida, tulishambulia kazi zilizokuwa zimebaki jana yake na kuzimaliza zote.

Tukaendelea kufanya kazi zote za siku hiyo ya jumamosi.

Ilipokaribia saa tano nilienda kuchukua diary yangu ili nienda katika kikao cha kila siku.

Tulipotoka katika kikaoni tukaunganisha kikao kingine cha pili.

Kawaida ya kila jumamosi panakuwa vikao viwili tofauti.

Kumbuka muda unasonga mbele bila kumngojea yeyote hapa duniani.

Ilipofika saa saba ikawa nimemaliza majukumu yangu yote ya siku hiyo.

Nilianza kijitayalisha kurudi nyumbani kwa mapumziko ya jummosi.

Nikawa napanga nikapate chakula cha mchana aina ya ugali na makange kule ninapoenda kula kila jumamosi.

Unajua ugali ukiwa wa moto na mboga ni rosti ya nyama yenye pilipili kwa mbali iliyochaganyika na mbogamboga na matunda ni Burudani sana.

Mara nikakumbuka kuwa watoto wanaitaji vitabu kwa ajili ya shule na leo nina nafasi ya kwenda kuwatafutia.

Nikachukua simu yangu nakumpigia  mama wawili  mke wangu ili afanye mambo mawili.

1. Aje kuchukua begi langu la ofisni hapo barabarani, kwani sitapitia nyumbani kwa wakati huo.

2. Anitumie  picha za vitabu vinavyotakiwa katika WhatsApp  yangu.

Nilitoka maeneo kazini na usafiri wangu  mpaka kituo cha mafuta  kilicho karibu.

Nilienda hapo hili kuongeza mafuta kidogo na kuangalia tairi za gari kama zina upepo Wa kutosha, kwa sababu ni siku nyingi sijaongeza upepo katka tairi zote.

Nilifanikiwa kuongeza mafuta tu Ila upepo haikuwezekana kwa sababu kulikuwa na foleni nami nikaona natachelewa kufika kariakoo.

Ilibidi niondoke hapo na kuendelea na safari yangu ya Kariakoo.

Nilipofika karibu na nyumbani nilimkuta mama wawili njiani akinisubiri, nilimpa begi langu nami nikaendelea na safari yangu ya Kariakoo.

Nilipofika maeneo ya tangibovu ilinibidi niingie kituo cha mafuta. Ili niongeze upepo tairi zote.

Zoezi ilo lilifanikiwa hapo katika kituo cha mafuta cha oil com

Safari ilianza hapo mpaka taa za kuongoza magari kona ya kuelekea kawe eneo la lugalo kambi ya jeshi.

Kituo cha pili kikawa taa za kuwavusha wanafunzi maeneo ya makongo.

Hapa kuna taa kwa ajili ya wanaotembea kwa mguu kuvuka njia nne bila shida.

Mtu yeyeto akiwa upande wowote anabonyeza kitufe na taa nyekundu inafuata ili nagari yasemame kuwapa watu fulsa ya kuvuka bila matatizo.

Kituo cha tatu kikawa taa za kuongoza magari njia nne mwenge kushoto kuelekea kiwanda cha soda cha cocacola na upande wa kulia ni kwenda mlimani city.

Tunapotoka hapo tukanyosha moja kwa moja

Kituo kilichofuata ni taa za kuongoza magari BamagaTBC. kona ya kwenda sinza na upande wa kushoto studio za TBC.

Tulipotoka TBC tukafika taa za kuongaza magari zamani palikuwa. panaitwa maji mchafu au sasa  sayansi TTCL hapo taa zilikuwa kijani  tukapita bila kusimama.

Unajua bahati uonekana mapema asubuhi nilipofika moroko kwenye njia panda kushoto ni kuelekea msasani na kulia kwake ni barabara ya kinondoni.

Mimi nikiwa natokea Mwenge naelekea mjini hapo tukanyosha moja kwa moja.

Kwa sababu taa za kutongoza magari zilikuwa kijani hakuna kusimama hapo moroko traffic light.

Tulipofika taa za Namanga kona ya kwenda msasani tulipunguza mwendo kidogo na kusimama hapo kwa sekunde chache.

Taa zilipowaka kijani tukaenda taratibu mpaka taa za kona ya kwenda kanisa katoriki saint peter. kwa bahati nzuri taa zilikuwa kijani.

Nilipita hapo kwa mwendo wa kawaida Kama ni dereva utanielewa tu.

Tulipofika mataa ya njia panda ya kwenda Kinondoni palikuwa na askari wa usalama barabarani yeye alikuwa akiyaongoza magari yaliyokuwa yanatoka upande wetu na upande wa mjini.

Hapo spidi ilikuwa ya wastani hivi kwa sababu magari yalikuwa karibu karibu.

Unajua macho yanapenda kuangali bahari

Eneo hilo upande wa mkono wa kushoto ni bahari .

Basi upande wa kushoto ukishapita taa za kuongoza magari kabla ya daraja la salender bridge kuna ujenzi unaendelea katikati ya bahari.

Unajua serekali ya awamu hii wanafanya kazi kweli kweli.

Mungu awape nguvu ya kutoangalia nyuma Ili wasonge mbele kuendeleza maendeleo nchi yetu yawe ya kimataifa na mfano kwa wengine.

Kuna kazi inaendelea ya ujenzi wa daraja kubwa la kisasa linalokatiza baharini lenye urefu wa kutosha linaloigharimu serekari mabilioni ya pesa.

Ni changamoto ya maendeleo katika karne hizi za sayansi na kiteknolojia kama zawadi kwa watanzania kwani daraja la kwanza lilijengwa mwaka 1929 na  kutumika kwa takribani miaka 51.

Ndipo mwaka 1980 serekali wakajenga daraja la pili lenye heshima yake kwa wakati huo.

Mnamo mwaka 2014 waziri wa ujenzi wakati huo Mweshimiwa Mgufuli alitangaza serekali inategemea kujenga daraja kubwa la kisasa maeneo ya salander bridge

Umeonaaa pale penye maendeleo ya kweli lazima utajikuta unatoa maelezo yasio na mwisho.

Mara kushtuka mataa ya salander bridges.
Kushangaa kote ningepitiwa na kunyosha kwenda katikati ya jiji.

Hapo tulisimama kwa dakika chache kwa sababu aliyekuwa akiongoza nagari ni askari wa usalama barabarani.

Ikanibidi nikae upande wa kulia barabara ya Alli Hassani mwinyi ili niweze kuingia barabara united nation.

Dakika chache tukawa  tumeingia Barbara ya umoja wa mataifa.

Njia ilikuwa nzuri kwangu , najua unasema kwanini.

Gari ya kwanza ilikuwa ya kwangu kwa hiyo nilikanyaga mafuta ili niwe wa kwanza kufika taa za fire zimamoto..

Katika taa zimamoto njia panda kushoto unaenda katikati ya jiji, kulia unaenda Magomeni.

Kwa wakati huo taa zikawa kijani hapo utata usipokuwa mjanja utabaki katikati.

Kwani taa za hapo zipo ruksa kwa wote .

Tukapita wote.

Mimi ikabidi niende mpaka maeneo ya kariakoo upandwe wa shule ya uhuru ili niweze kupata parking ya uwakika.

Nilipata sehemu ya kupaki Gari ambopo uwa napaki kila niendapo Kariakoo.

Kama nilivyokupasha hapo nyuma nia yangu ya kuja huku ni kutafuta vitabu vya watoto.

Hiyo siku ilikuwa ni siku yangu ya kutembea nilitembea kupita kiasi.

Hapa nawasubiria google watoe timeline yangu ya mwezi wa tisa ili nione mzunguko wangu ulikuwaje.

Wakati Natoka Kariakoo sokoni kuelekea mzunguko wa msmbazi.

Nikiwa maeneo ya jengo DDC karikooo gafla kwa mbele mama mmoja aliyekuwa amembeba mtoto mdogo alianguka huku mtoto akiwa mikononi mwake.

Alipokuwa anatembea hapo bahati mbaya akalanyaga banda la ndizi na kuteleza akaanguka chini.

huyo mama alikuwa amefuatana na watoto wake wa kiume wawili si wakubwa sana Ila ni Kati ya miaka kumi na mwingine nane hivi.

Yule kijana mkubwa akakimbilia mama Yake na kumbeba yule mtoto mdogo ambaye wakati uo alikuwa akilia kwa sauti kubwa.

Watu waliokuwapo eneo hilo hakuna hata mmoja aliyejaribu kumpa msaada yule mama kwa muda wote.

Mungu akanipa nguvu nilikimbilia pale na kupata nguvu ya kuwasogeza watu waliomzunguka yule mama wakimshangaa bila kutoa msaada wowote.

Huwezi amini yule mama alikuwa hawezi tembea ananyonga mguu kwa maumivu makali na kulia kama mtoto mdogo.

Mungu akanimbia wewe ni mwanajeshi kwa wakati huu onesha nguvu yangu kupitua kwako.

Basi niliinama na kumuambia yule mama nipo hapa kwa ajili yako sima nikumbatie mimi begani ili nikupeleke pembeni kwani hapo upo njiani na watu ni wengi watakukanyaga.

Mungu ni wa ajabu nilipata nguvu nikamtoa yule mama pale njiani na kumuweka pembeni ya jengo la DDC karibu na duka moja lililokuwa wazi.

Nikamuliza yule mama nini tufanye au tumpeleke hospital.

Kabla ya ajato jibu swali lingine kwa yule mama
Unaishi wapi hapa Dad es salaam.

Yule mama akajibu mtoni kijichi

Daa ni mbali toka hapa tulipo Kariakoo.

Bila kupoteza muda pembeni yetu wapo madereva wa tax...

Nikamfuata mmojo wa wale madereva

Nilipomueleza kuna mgonjwa anaitaji msaada kupelekwa hospital iliyo karibu na anapokaa mtoni.

Yule dereva akaondoka bila jibu , alipokuwa akiondoka akaenda kuongea na mwenzake .

Naye alipokuja akaja na vikwazo vya kumwacha njiani kwani hiyo ni kesi.

Akili yangu ikakumbuka bajaji ndipo nilipouliza zipo wapi! walio karibu yangu wakainua kichwa kuangalia upande wa pili wa barabara ya msimbazi.

Ndipo nilipoanza kukimbia kuelekea sehemu  bajaj zilipopaki.               

Nilipofika hapo nikaanza kupatana bei ya kutoka kariakoo mpaka mtoni kijichi.

Ndipo dereva wa bajaji akakubali kwa elfu kumi na tano.

Nakumbuka nilimuambia nifuate huku.

Mimi nikatoka mbio kuelekea kwa mgonjwa wetu

Bajaj ilipfika nikamuomba mama mmoja aliyekuwepo katika eneo hilo kumnyanyua ili tupeleke katika bajaji.

Kawaida msimbazi eneo la DDC uwa na watu wengi kwa nyakati za mchana tens siku za jumamosi.

Ilibidi nipangue njia kwa sauti kubwa Sogea sogea kama mimi mwanajeshi sauti yangu ilisikika kaa pembeni pisha pisha  sogea wewe vipi kaa pembeni.

Na mungu ni mwenye nguvu watu wanasogea bila ubishi mpaka na wengine mpaka wajeuke nyuma wakimuoa yule mgonjwa wanapisha pembeni

Yule mama kwa mbali niliskia akisema asante Sana Mungu atakubaliki

Basi vitabu venyewe sikuvipata Ikabaki kurudi nyumbani.

Kama una maoni yoyote

kimarokenny@gmail.com au

+255769922003

Mwisho.

Kennedy Kimaro

Tuesday, July 9, 2019

VIFO VILIVYOTOKEA KWA WANA HABARI WA AZAM MEDIA

Sipati picha kwa majonzi yaliyomo ndani ya moyo wangu kutokana na ajali, iliyosababisha vifo vya watu saba miongoni mwao wafanyakazi watano wa Azam Media.

Najaribu kuvuta picha kwa vijana mafundi wachapakazi hodari jinsi ndoto zao na mipango yao katika taasisi ya habari chini ya movuli Azam Media Group.

Maisha ni sawa na universe ilivyo na umbo kubwa  na umbali husiogawanyika na namba yeyote.

Unaanza mipango yako vizuri bila woga lakini huwezi tazama mbele kuna nini.

Nikijaribu Najaribu kuinua macho yangu juu na kupeleka fikra zangu za ujana kwa vijana wenzangu Azam Media.

Basi nabaki katikati ya fikra na kunyamaza kimya huku simanzi za machozi zikinijia kwa mbali.

Maswali mengi yamejikita katika fikra za ubongo wangu kutokana na tukio hilo la ajali.

Mawazo mengi yanakuja mbele yangu, lakini sipati picha katika fikra zangu, nini kilichotokea na kupelekea kubaki kimya.

Sisi ni binadamu na yale yote yaliyotokea  tunayaona sisi tuliobaki  hapa duniani.

Lakini vijana hawa.

1. Salim J Mhando
2. Silvanus W Kassong
3. Charles Wandwi
4. Florence B Ndibalema
5. Said H Hassan

Tuwawashia mishumaa ya maombolezi kwa wote watano

Safari yao ya hapa duniani ndio imefika mwisho.

Majonzi na maumivu ya simanzi zinabaki kwetu tulio hapa duniani.

Nashindwa kuendelea kuandika chochote zaidi ya kuwaombea wale wote waliofariki.

Nanyamaza kimya na kuangalia dunia inavyo songa mbele kwa spidi.

Na
Kennedy Kimaro.

Wednesday, June 26, 2019

MTAZAMO WANGU KAMA MKAZI WA EAST AFRIKA.

Watu wenye tabia za ubaguzi na umimi kama hawa ni hatari sana. 

Dunia imekuwa kama kijiji katika karne hii kutokana na ushirikiano wa  kisayansi na teknolojia.

Inapelekea watu kuingia kona zote za dunia ili wawekeze na kutafuta kazi za kufanya kupata kipato na kuongeza kasi ya maendeleo na uchumi kupata nguvu ya  kusonga mbele.

Hapo inapelekea binadamu kujichanganya katika jamii mbali mbali na kusababisha wakenya kuweza kuchumbia au  kuoa mtanzania au mganda, vivyo hivyo kwa waganda na watanzania na dunia nzima.

Tena sio east Afrika tu, watu wanaoana toka sehenu mbalimbali hapa duniani mifano middle east, Europe, Asia, Russia, America

Ukianza kuwabagua wengine na kujifanya nyie ndie mwenye Fulsa ya  kustahili kupata kitu au haki fulani, hiyo tabia ni hatari sana katika kizazi hiki cha sayansi na teknolojia.

Chuki za namna hii ni sawa kupanda mizizi ya magugu maji katika maisha ya binadamu.

Ukiwa na tabia ya chuki na ubaguzi kama hii ni hatari sana, haiwezi ishia hapo. itaendelea kwa vizazi na vizazi.

Baadaye uacha picha yenye mfano mbaya kwa watoto wetu.

Tabia kama hizi zikijitokeza lazima zikemewe mara moja.

Tabia kama hizi zinajenga uchochezi utaokufanya  kesho kuanza kuwabagua hata ndugu unawaona sio wa karibu yako..

Siasa za namna ni hatari  sana katika jamii zetu na kizazi cha vijana wa sasa.

Tumpe sifa Nyerere kwa kutuepusha na mambo kama hayo.

Sisi wabongo hapa kazi tu.. njoo na fedha zako.

Wekeza kwetu ili uongeze ajila kwa watanzania.

Tunajikita katika sera za kuongeza viwanda katika nchi yetu bila ubaguzi kwa raia yeyote kutoka mahali popote.

Kinachotakiwa uje na sifa za kuwekeza ili uchumi wetu upande juu.

Hiyo ndio Tanzania ya sasa yenye picha ya maendeleo kwa wote.       😄🥺👆

Wako @Kimaro.

Wednesday, June 6, 2018

SAFARI YA MAPACHA MARIA NA CONSOLATA 1996 MPAKA 2018

JAMANI MAISHA NI HADITHI YENYE STORI INAYOANZA BILA WEWE KUJUA NA INAISHA BILA WEWE KUJUA.

KWANZA JIULIZE WEWE UPO UPANDE GANI WA HADITHI HII KATIKA MAISHA YAKO KILA SIKU.

PILI JIULIZE KUNA USHAWISHI WOWOTE ULIFANYIKA ILI UZALIWE KATIKA FAMILIA ULIYOPO SASA.

JIBU LITAKUWA HAPANA ILA MUNGU NDIYE ANAYEPANGA YOTE YAFANYIKE.

MUNGU ALI MUUMBA MTU AKASEMA NA TUMFANYE MTU KWA MFANO WETU. KWA SURA YETU.
WAKATAWALE SAMAKI WA BAHARINI NA NDEGE WA ANGANI NA WANYAMA NA NCHI YOTE PIA.

HAPO NDIPO HADITHI NZURI YA MAISHA ILIPOANZA NA KUSABABISHA KIZAZI KU- TAWANYIKA DUNIANI KOTE.

HAPO MAISHA YAKAANZA NA KUKAWA NA WATU WENYE MUONEKANO TOFAUTI KUTOKA NA MAENEO WALIYOKUWA.

MAISHA YAKAWA YAPO YAKASABABISHA WATU KUWEPO KWA WAKATI NA YENYEWE YANAENDELEA TU DUNIANI.

MIMI NIPO NA NAMSHUKURU MUNGU KWA KUNIPA NAFASI MPAKA SASA.

UNAMSHUKURU MWENYEZI MUNGU KWA KUKUPA NAFASI YA KUENDELEA KUWEPO MPAKA SASA.

SASA TUTAZAME NINI KILICHONISABABISHA  KUYAANDIKA HAYA MACHACHE KWAKO.

MNAMO MWAKA 1996 MAMA MMOJA TOKA  MKOANI IRINGA WILAYA YA MAKETE ALIBEBA MIMBA KWA MIEZI TISA KAMA KAWAIDA YA WANAWAKE.

ILIPOFIKA MUDA WA KUJIFUNGUA KAMA WAZAZI WENGINE.
NDIPO  ALIKWENDA KATIKA HOSPITALI YA MISHENI IKONDA MKOANI IRINGA ILI KUPATA HUDUMA ZA UZAZI..

ALIJIFUNGUA WATOTO MAPACHA WAWILI WALIOUNGANA MWILI.

HADITHI YA WATOTO WAWILI WALIOUNGANA ILICHOMOKA HAPO NA WATOTO KUPEWA MAJINA YA MARIA NA CONSOLATA MNANO MWAKA 1996.

KANISA LILIWACHUKUA MARA MOJA MARIA NA CONSOLATA WAKAWA CHINI YA SHIRIKA LA KIKRISTO.

CHA KUPENDEZA KWA AKINA MARIA NA CONSOLATA WALIJIONA WAPO SAWA NA WATU WENGINE.

MAISHA YAO YA KUKUBALI MATOKEO ULEMAVU WAO MOYONI NDIO  UWEZO NAFSI YA IMANI  WALIYOPEWA NA MWEYEZI MUNGU.

MSIMAMO WA KUENDELEA NA MICHAKATO KUENDELEA  KUJIKITA KATIKA VITU VYA KIDUNIA.
IJAPOKUWA WAO NI WALEMAVU NI FUNDISHO KWETU LISILOKUWA NA MFANO.

MUNGU ALIWAPA MARIA NA CONSOLATA HEKIMA NA UWEZO WA KUWA WALIMU NA KUTUACHIA MFANO KWETU KUTOKANA NA MATENDO YAO.

INGAWA LEO HAWAPO TENA DUNIANI LAKINI BADO TUTAWAKUMBUKA.

BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA
WAPUMZIKA KWA AMANI.

KENNEDY MARO

Sunday, May 27, 2018

Mafunzo ya imani kwa binadamu kwa kuubiri ukweli.

Mara nyingi napenda kusikiliza maubiri ya neno la Mungu toka kwa wachungaji tofauti hapa duniani.



Lakini napenda mchungaji anayetumia maandiko ya biblia kama nguzo yake ya kuubiri amani.



Mungu ambariki na kuwaonyesha njia watumishi wake walio wengi kulisambaza nene lake. 



Ndio maana roho mtakatifu aligawa nguvu za lugha tofauti ili neno lisambae duniani kote.



Kazi ya kulisambaza neno la Mungu pande zote duniani ni kazi ya kila mmoja wetu.



Kuna kitu kimoja ambacho kinanionya kutojaji imani ya dini ya binadamu mwingine yeyote, kwa sababu yeye au mimi tuna utashi wa kuwa upande wa imani wowote bila kulazimishwa na mtu yeyote.



Imani ni njia ya binadamu kujenga mahusiano kati yake na Mungu.



Imani ndio njia yenye nafasi ya matumaini kwa kila mtu kufanya mahamuzi ya kujijenga katika mahusiano yenye ushawishi wa nafsi yake na Mungu.



Tulipewa nafsi yenye imani ili kulitangaza neno lake Mungu kutoka katika masoma au mafundisho yaliyopo katika vitabu vitakatifu katika biblia.



Vitabu vitakatifu vinavyotumika kufundisha yale yaliyo na hekima ili kutufungulia upendo wa kweli toka kwa Yesu kristo.



Upendo wa mafundisho ya Yesu kristo ni njia yenye mafunzo yake kwa upeo na busara na amani.



Yesu alikuja na kutufundisha yale yaliyo mema ili kutufungulia njia ya faraja katika safari ngumu hapa duniani.



Mafundisho yake yote yalikemea mabaya na kukataa kurudia maneno mabaya.



Mungu alikemea matendo mabaya kwa kutufundisha kutenda yaliyo mema.



Mfano kitabu cha waamuzi mlango wa 13 kinatufundisha hivi...



MLANGO 13



1 Wana wa Israeli wakafanya tena yaliyo mabaya mbele za macho ya Bwana, Bwana akawatia katika mikono ya Wafilisti, muda wa miaka arobaini. 



2 Palikuwa na mtu mmoja wa Sora, wa jamaa ya Wadani; jina lake akiitwa Manoa; na mkewe alikuwa tasa, hakuzaa watoto. 



3 Malaika wa Bwana akamtokea yule mwanamke, akamwambia, Tazama, wewe sasa u tasa, huzai; lakini utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanamume. 



4 Basi sasa, jihadhari, nakuomba, usinywe divai wala kileo, wala usile kitu kilicho najisi; 



5 kwani tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanamume; na wembe usipite juu ya kichwa chake; maana mtoto huyo atakuwa mnadhiri wa Mungu tangu tumboni; naye ataanza kuwaokoa Israeli na mikono ya Wafilisti. 



6 Ndipo yule mwanamke akaenda akamwambia mume wake, akisema, Mtu wa Mungu alinijia, na uso wake ulikuwa kama uso wa malaika wa Mungu, wa kutisha sana; nami sikumwuliza, Umetoka wapi? Wala hakuniambia jina lake; 



7 lakini aliniambia, Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanamume; basi sasa, usinywe divai wala kileo, wala usile kitu kilicho najisi. Maana mtoto huyo atakuwa Mnadhiri wa Mungu tangu tumboni, hata siku ya kufa kwake. 



8 Ndipo huyo Manoa akamwomba Bwana, akisema, Ee Bwana, nakuomba, yule mtu wa Mungu uliyemtuma na aje kwetu mara ya pili, atufundishe hayo yatupasayo kumfanyia huyo mtoto atakayezaliwa. 



9 Mungu akasikiza sauti ya Manoa; naye malaika wa Mungu akamwendea yule mwanamke tena alipokuwa anaketi shambani; lakini mumewe, Manoa, hakuwapo pamoja naye. 



10 Basi huyo mwanamke akaenda haraka, akapiga mbio, na kumwambia mumewe, akisema, Tazama, huyo mtu amenitokea, huyo aliyenijilia siku ile. 



11 Basi Manoa akainuka, akamwandama mkewe, na kumfikilia mtu huyo, akamwuliza, Je! Wewe ndiwe mtu yule aliyenena na huyu mwanamke? Akasema, Naam, ni mimi. 



12 Manoa akasema, Basi sasa hayo maneno yako yatakapotimia, je! Huyo mtoto atakuwa wa namna gani, na kazi yake itakuwa ni nini? 



13 Malaika wa Mungu akamwambia Manoa, Katika hayo yote niliyomwambia huyo mwanamke na ajihadhari. 



14 Asile kitu cho chote kitokacho katika mzabibu, wala asinywe divai, wala mvinyo, wala asile kitu cho chote kilicho najisi; hayo yote niliyomwamuru na ayatunze. 



15 Kisha Manoa akamwambia huyo malaika wa Bwana, Nakuomba, tukuzuie, ili tupate kuandaa mwana-mbuzi kwa ajili yako. 



16 Lakini malaika wa Bwana akamwambia Manoa, Ujapokuwa wanizuia, sitakula katika mkate wako; na kwamba wataka kufanya tayari sadaka ya kuteketezwa, inakupasa kumsongezea Bwana. Kwa kuwa Manoa hakujua ya kwamba yeye ni malaika wa Bwana. 



17 Manoa akamwambia huyo malaika wa Bwana, Jina lako ni nani, ili kwamba hapo hayo maneno yako yatakapotimia nipate kukutukuza? 



18 Huyo malaika wa Bwana akamwambia, Kwani wewe kuniuliza jina langu, kwa kuwa jina hilo ni la ajabu? 



19 Basi Manoa akamtwaa yule mwana-mbuzi, pamoja na sadaka ya unga, akamtolea Bwana hapo juu ya mwamba; huyo malaika akatenda la ajabu; Manoa na mkewe wakaangalia. 



20 Kwa maana, ikawa, mara huo mwali wa moto ulipopaa juu mbinguni kutoka pale madhabahuni, huyo malaika wa Bwana akapaa katika mwali wa moto wa madhabahu; nao Manoa na mkewe wakaangalia; wakainama kifudifudi. 



21 Lakini malaika wa Bwana hakumtokea Manoa tena, wala mkewe. Ndipo Manoa alipojua ya kwamba ndiye malaika wa Bwana. 
22 Manoa akamwambia mkewe, Hakika yetu tutakufa sisi, kwa sababu tumemwona Mungu. 



23 Lakini mkewe akamwambia, Kama Bwana angetaka kutuua hangepokea sadaka ya kuteketezwa, wala sadaka ya unga, mikononi mwetu, wala hangetuonyesha mambo hayo yote, wala hangetuambia mambo kama hayo wakati huu. 



24 Basi yule mwanamke akamzaa mtoto mwanamume akamwita jina lake Samsoni

Friday, April 6, 2018

IMANI ILIYO NA UPENDO

UPENDO UNAOTOKA KWA MTU NI TABIA YA NAFASI KATIKATI MOYO WAKE.
UPENDO SIYO KITU CHA KULAZIMISHA. UPENDO NI  IMANI ILIYO YA KWELI KATI YAKO NA MUNGU.

Sunday, February 18, 2018

Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu.

MLANGO 20

1 Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu.

2 Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu

3 Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi; 

4 na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda.
 
5 Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile. 

6 Hata kama saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi? 

7 Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, enendeni nanyi katika shamba la mizabibu
 
8 Kulipokuchwa, yule bwana wa shamba akamwambia msimamizi wake, Waite wakulima, uwalipe ujira wao, ukianzia wa mwisho hata wa kwanza. 

9 Na walipokuja wale wa saa kumi na moja, walipokea kila mtu dinari

10 Na wale wa kwanza walipokuja, walidhani kwamba watapokea zaidi; na hao pia wakapokea kila mtu dinari

11 Basi wakiisha kuipokea, wakamnung'unikia mwenye nyumba, 

12 wakisema, Hao wa mwisho wametenda kazi saa moja tu, nawe umewasawazisha na sisi tuliostahimili taabu na hari za mchana kutwa.

13 Naye akamjibu mmoja wao,
akamwambia, Rafiki, sikudhulumu; hukupatana nami kwa dinari

14 Chukua iliyo yako, uende zako; napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe. 

15 Si halali yangu kutumia vilivyo vyangu kama nipendavyo? Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa mwema?

16 Vivyo hivyo wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho

Saturday, February 17, 2018

Tuesday, September 12, 2017

https://youtu.be/tirS_O1uVyw

Sunday, September 3, 2017

Monday, July 24, 2017

Maisha ya vijana katika jiji la Makonda Dar es Salaam.

Maisha ya leo ni tafu Kwa vijana wa leo.
Najua unanishanga kunisikia nikisema jinsi nilivonena hapo juu.

Wewe Mtanzania tazama jinsi ulivyo kama wewe unavyo starehe kwa kujikimu na kutatua ukata wa maisha hapa ndani ya jiji la Makonda.

Najaribu kuvuta picha na kuangalia jinsi ya maisha yetu yalivyogawanyika katika tabaka mbalimbali zenye tofauti ya maslahi.

Kabla ya kujikita katika gumzo na stori iliyopita mbele ya macho yangu na kuniweka katika tabaka la mawazo.

Najaribu kukuvuta mawazo yangu, ili nawe ufanye utafiti wenye njia iliyo na mistari sambamba yenye kukuonesha miangaiko wanayopitia wasio na uwezo katika jiji la Makonda.

Najua mawazo yako yatakimbilia kwa maskini walio wengi wanajulikana kama ombaomba wa mitaani.

Funga na fungua macho yako katika mtazamo wenye fikra zenye wigo mpana.

Tazama kwa umakini mkubwa kuwa jamii yenye umaskini si ombaomba tu.

Kuna watoto wengi wanaishi katika mazingira mgumu duniani kote.

Kuna watoto wanaofanyishwa kazi ngumu majumbani na maeneo yenye vita za wenyewe kwa wenyewe.

Tupia jicho lako utazame watoto wanaozaliwa na kutopewa malezi na wazazi wao na kupelekea kuwa watoto wa mitaani.

Jaribu kuvuta picha na kuangalia jinsi ya familia maskini katika maisha ya kila siku jinsi wanayopata taabu za chakula nguo na mahitaji yao kwa ujumla.

Tazama maisha yako na uleule upande wa pili tupia jicho kwa familia maskini.

Jitazame chai yako ya asubuhi gharama yake ni shilingi ngapi!

Jitazame chakula chako cha mchana Chips kuku na vingine vya thamani bei yake ni kiasi gani.

Tazama wangapi wanakwenda kunachangia mchango angalau kidogo kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu.

Jaribu kuelewa ni nani mchango wako katika familia zisizojiweza katika maisha yao kila siku.

Ebu twende na mimi bega kwa bega upate kujua kipi ninacho.

Jumapili nikiwa katika gari eneo la Mataa ya kuelekea Msasani, wakati huo taa nyekundu zimewaka upande wetu.

Magari yanayotokea mjini kuelekea msasani yalikuwa yanapita,  upande mwingine kuna mistari ya pundamilia ya watembea kwa miguu kukatiza barabara.

Kukawa na kijana mmoja ukimtizama utamuona ni wa kawaida tu.
Cha ajabu uyo kijana mawazo yake hayakuwepo pale alipo.

Basi yule kijana akawa anavuka barabara bila ya kujali kuna gari linakuja au vipi?

Kufumba na kufungua gafla gari ikafungwa breki miguuni kwa yule kijana.

Ikabidi arudi nyuma ili gari lipite, tulipo mwambia kulikoni ndugu yetu huna macho.

Yule kijana akajibu ni maisha ndio yanafanya hivi.

Hapa tangu asubuhi sijaonja chochote kinywani.

Mchana umeshapita naungalia hivi hivi.

Kingine kinachonitesa hapa kwamba sijui nitafika vipi Mbagala wakati nipo msasani na sijui nipo katika dunia hii au vipi.

Sina hata sentano hapa mfukoni, ni taabu na shida katika maisha yangu.

Nakumbuka mimi ndio gari ya kwanza mbele, niliyaona yote yakitokea

Basi haraka nikatoa shilingi elfu moja na kumpa yule kijana.

Sikutegemea kitu alichokuwa akifanya yule kijana.
Alipiga magoti na kunishukuru huku machozi yakimtoka na akionyesha mikono juu kumshukuru Mungu.

Wakati huo taa za barabarani zinawaka kijani nasi tuliondoka.

Lakini njiani nikawa na uchungu wa moyo

Itaendelea
Wako
Kennedy Kimaro

Friday, July 21, 2017

Maisha ya vijana wa sasa.

Ebu tubige stori fupi  kidogo ya maisha ya vijana wa sasa.

Kila asubuhi baada ya kujiweka sawa kwa safari ya kibaruani.
Nilipata chai ya asubuhi kama kawaida. Nikabeba simu zangu mbili na funguo za gari yangu.

Nilitoka nje ya nyumba yangu kuelekea kwenye gari yangu.

Mama watoto na watoto wakaja kunifungulia Gqeti kama kawaida yao.

Wakati ninarudi nyuma na gari, uku niki seti redio station moja ili kupata taarifa za kila siku.

Kukawa na watangazaji katika kipindi kimoja cha asubuhi wakitafakari yaliyondikwa kwenye magazeti ya siku hiyo.

Kikubwa kilikuwa ni mwanasheria ambaye ni mwana siasa wakati alipogoma kutoka ndani ya mahakama kuepushwa kukamatwa na polisi.

Wakati huo mtangazaji mmoja a akitoa stori ya kibaka au mwizi sugu aliyekimbizwa mitaa ya kawe na kufananisha suala la yule mwanasiasa

Stori ilianza hivi, yule mwizi alipokuwa akakimbizwa na raia wenye uchungu wa kuibiwa kila mara nyakati za usiku wa manane.
Wakawa wanamkimbiza yule mwizi kimya kimya ili wamshikishe nidhamu ya kutorudia tabia ya wizi.

Yule mwizi kwa mwendo kasi akakatiza karibu na kituo cha polisi cha kawe.

Alipoangalia kwa mbele akawaona askari wamesimama eneo la mapokezi.

Moyoni akasema liwalo na liwe maisha ni matamu, nikipoteza muda nitapata kichapo cha nguvu na kupoteza maisha hapa.

Basi yule mwizi akaongeza mwendo kuelekea upande walipo askari polisi kituo cha kawe eneo la mapokezi na kusima nyuma yao.

Mtangazaji akaendelea kusimulia stori ya kibaka mwizi sugu.

Ndipo wale raia wema ilibidi wasimame gafla kwa kutoamini nini kilichotokea hadi mwizi kukimbilia upande wa kituo cha polisi.

Wale raia wema wakashauliana mmojawapo aende kuchukua yule mwizi sugu toka mikononi mwa polisi.

Ndipo njemba mmoja alichomoka na kuelekea alipo mwizi sugu katika kituo cha polisi.

Alipofika katika eneo ambapo yule mwizi mwizi chini ya ulinzi wa askari polisi 

Askari polisi wakamuliza yule raia mwema? Una shida gani kijana!

Naye akamjibu, nimekuja kuchukua ndugu yangu huyo hapo

Huyu ndugu yetu ana matatizo ya akili siku nyingi.

Kwa sauti kubwa yule mwizi akajibu, Muongo Muongo mimi ni mwizi na wanataka kuniua.

Wakati polisi wakiwa katika mshangao kwa yote yanayotokea

Mara yule raia mwema akawa anajeuka upande mwingine ili kurudi nyuma gafla chuma kizito kikaanguka kutoka mfukoni mwake.

Basi yule mwizi akasema unaona askari chuma alichobeba anataka kuniua huyu.

Kumbe yule mwizi naye anajua kazi ya askari ni kuleta amani pale palipo na machafuko.

Kazi ya  askari kusikiliza pande zote mbili zenye malalamiko ili kufanya uchunguzi na kujua nani ni mkosaji.

Askari alichofanya ni kuwakamata wote wawili na kuwakilisha chini mapokezi kwa muda.

Najua unanishanga Kwanini wote wawili na si akamatwe yule mwizi sugu.

Wakati huyu ni mwizi na amekuwa akifanya wizi  leo na siku zote za ujana wake.

Yule askari akaja na karatasi za kuandika ripoti ya kesi iliyopo mbele yake.

Wa kwanza kuitwa kutoa maelezo yake ni yule  mwizi sugu kwa yeye ndiye wa kwanza kufika kituo cha polisi.

Askari akaanza.. Unaitwa nani ndugu yangu.

Mwizi akajibu.. Naitwa... .

Una miaka mingapi!

Mwizi akajibu kumi na saba!√

Unaishi wapi

Mwizi akajibu kivukoni!

Kwanini umekuja hapa katika kituo cha polisi!

Mwizi..  Kimya

Askari akamgeukia tena yule mwizi sugu na swali lile lile.

Mwizi Sugu Kimya tena.. 

Basi askari polisi  akumweleza kama huna jibu basi nitakukabizi kwa ndugu yako.

Yule mwizi sugu akajibu

Wataniua Watamuua.. Huyu siyo ndugu yangu kwanza simjui huyu huku akilia

Ndipo yule askari polisi akamuuliza swali lile mara ya tatu

Mwizi akajibu

Yeye ni mwizi na kazi zake mchana ni

mpiga debe wa daladala na usiku wanajikusanya na kuiba katika nyumba za watu au vifaa katika magari.

Askari akamwambia weka sahihi yako katika maelezo haya.

Mwizi sugu akachukua peni na kumwaga wino au sahihi katika maelezo yake.

Askari akamchukua na kumweka ndani mpaka siku inayofuata.

Jaribu kuwaza askari polisi alifanya maamuzi gani kwa yule raia mwema.

Mwisho
Kennedy Kimaro
@kennedytz2

Tuesday, July 11, 2017

Mtu aliye mzushi, baada ya kumwonya mara ya kwanza na mara ya pili, mkatae; 

Lakini wema wake Mwokozi wetu Mungu, na upendo wake kwa wanadamu, ulipofunuliwa, alituokoa; 

si kwa sababu ya matendo ya haki tuliyoyatenda sisi; bali kwa rehema yake, kwa kuoshwa kwa kuzaliwa kwa pili na kufanywa upya na Roho Mtakatifu; 
ambaye alitumwagia kwa wingi, kwa njia ya Yesu Kristo Mwokozi wetu; 

ili tukihesabiwa haki kwa neema yake, tupate kufanywa warithi wa uzima wa milele, kama lilivyo tumaini letu. 

Ni neno la kuaminiwa; na mambo hayo nataka uyanene kwa nguvu, ili wale waliomwamini Mungu wakumbuke kudumu katika matendo mema. Hayo ni mazuri, tena yana faida kwa wanadamu. 

Lakini maswali ya upuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana. 

Mtu aliye mzushi, baada ya kumwonya mara ya kwanza na mara ya pili, mkatae; 

ukijua ya kuwa mtu kama huyo amepotoka, tena atenda dhambi, maana amejihukumu hatia yeye mwenyewe. 

Sunday, July 2, 2017

Ikawa usiku uo huo, neno la Bwana likamfikia Nathani kusema

Nathani akamwambia mfalme, Haya, fanya yote yaliyomo moyoni mwako; maana Bwana yu pamoja nawe.

Ikawa usiku uo huo, neno la Bwana likamfikia Nathani kusema,

Enenda, ukamwambie mtumishi wangu, Daudi, Bwana asema hivi, Je! Wewe utanijengea nyumba, nikae ndani yake?

Kwa maana mimi sikukaa ndani ya nyumba, tangu siku ile niliyowatoa wana wa Israeli katika Misri, hata leo, lakini nimekaa katika hema na maskani.

Saturday, July 1, 2017

Kwa maana, ndugu mnaopendwa na Mungu, twajua uteule wenu.

Wala hatuachi kuikumbuka kazi yenu ya imani, na taabu yenu ya upendo, na saburi yenu ya tumaini lililo katika Bwana wetu Yesu Kristo, mbele za Mungu Baba yetu.

Kwa maana, ndugu mnaopendwa na Mungu, twajua uteule wenu;

Thursday, June 29, 2017

SIPATI PICHA NA MATUKIO YA KIBITI

Mimi kama mwananchi wa kawaida ndani ya nchi yangu Tanzania.

Najaribu kuvuta taswira ya matukio yanayoendelea kutokea ndani ya nchi yetu Tanzania pande za Kibiti.

Tutazame katika upande wa imani zaidi kuliko kuanza kuhukumu kila mtu.

Ebu tuangalie ni nani anayetenda mambo haya, yasiyokuwa na mwelekeo katika tabia mila na tamaduni za kitanzania.

Mtazame huyu Mtanzania mwenye makabila zaidi ya mia na kitu.

Huyu Mtanzania aliye zaliwa na kukua Katika desturi za mchanganyiko wa makabila mbalimbali yanayofundisha malezi yenye kuheshima.

Huyu Mtanzania aliyesoma katika shule zenye mchanganyiko wa makabila na jinsia tofauti.

Huyu  Mtanzania aliyesoma lugha ya Kiswahili kama lugha moja ya mawasiliano kwa wote.

Huyu Mtanzania, huyu Mtanzania anayeishi katika nchi yenye amani, yenye upendo na ukarimu kwa wageni.

Huyu Mtanzania mwenye umoja wa kitaifa uliojengwa na baba wa taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Nyakati hizo Nyerere alijenga umoja wa kitaifa kwa watanzania kupitia vijiji vya ujamaa na kujitegemea.

Hapa kilizaliwa kitu kinaitwa nguvu kazi kwa kila raia wa kawaida.

Wenye elimu zao, walifanya kazi katika serikali na mashirika mengine binafsi.
Yote ni kusukuma gurudumu la maendeleo kwa wananchi wa kawaida.

Wewe Mtanzania amka sasa na fungua macho yako, tazama mbele kwa umakini ili uepushe hizi uchocheezi wa kibaguzi.

Unaofanywa na wauaji wa raia wa tanzania kwa tamaa au chuki binafsi zinazoendelea kunyesha na watu wachache.

Tambua kile ambacho kinachoonekana sasa kama mauaji ya raia wenye haki ni hatari kwa kizazi hiki na kinachokuja.

Tambua yanayoendelea kupoteza haki kwa wenye haki na wasio na hatia ni kinyume na haki za binadamu duniani kote.

Jenga imani yako kwa kujenga upendo kwa wote

Kemea chuki yako uliyoijenga katika fikra zako kwa kuwaua wenye haki.

Jaribu kuitupa hiyo chuki yako mbali kama maandiko haya chini...

Achukiaye huficha chuki kwa midomo yake; Naye huweka akiba ya hila moyoni mwake. 

Anenapo maneno mazuri usimsadiki; Kwa maana ana machukizo saba moyoni mwake. 

Ingawa chuki hufunikizwa kwa hila; Uovu wake utadhihirika mbele ya kusanyiko. 

Achimbaye shimo atatumbukia mwenyewe; Naye abingirishaye jiwe litamrudia.

Kama ulipewa uhai na muumba wa mbingu na nchi,  basi basi kumbuka nawe ipo siku yako ya mwisho kama unavyo fanya kwa wengine wenye haki ya kuishi kama unavyoishi wewe.

Kazi ya shetani ni kuibomoa imani na kuupoteza ufalme wa Mungu.

Naye asema hivi..

Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. 

Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. 

Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. 

Tusimame kama watoto wa Baba na Mtanzania mwananchi wa kawaida mwenye upendo na nchi yake.

Kwa pamoja tutokomeze ili janga kubwa linalo chepukia katika maadili yetu.

Tusipo kemea na kulipinga leo, kesho litakuwa ni chaka kubwa la mateso kwetu.

Wenu
Kennedy Kimaro
www.kennedytz.blogspot.com

Sunday, June 25, 2017

ANGALIENI MTU AWAYE YOTE ASIMLIPE MWENZIWE MABAYA KWA MABAYA

Kwa kuwa Mungu hakutuweka kwa hasira yake, bali tupate wokovu, kwa Bwana wetu Yesu Kristo; 
10 ambaye alikufa kwa ajili yetu, ili tuishi pamoja naye, kwamba twakesha au kwamba twalala. 
11 Basi, farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake, vile vile kama mnavyofanya. 
12 Lakini, ndugu, tunataka mwatambue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu, na kuwasimamia ninyi katika Bwana, na kuwaonyeni; 
13 mkawastahi sana katika upendo, kwa ajili ya kazi zao. Iweni na amani ninyi kwa ninyi. 
14 Ndugu, twawasihi, waonyeni wale wasiokaa kwa utaratibu; watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote. 
15 Angalieni mtu awaye yote asimlipe mwenziwe mabaya kwa mabaya; bali siku zote lifuateni lililo jema, ninyi kwa ninyi na kwa watu wote. 

UFALME WA MUNGU HAUJI KWA KUCHUNGUZA

Na alipoulizwa na Mafarisayo, Ufalme wa Mungu utakuja lini? Aliwajibu akawaambia, ufalme wa Mungu hauji kwa kuuchunguza; 
wala hawatasema, Tazama, upo huku, au, kule, kwa maana, tazama, ufalme wa Mungu umo ndani yenu. 

Thursday, June 22, 2017

Huwapamba wenye upole kwa wokovu.

Na walisifu jina lake kwa kucheza,
Kwa matari na kinubi wamwimbie.
Kwa kuwa Bwana awaridhia watu wake, Huwapamba wenye upole kwa wokovu.

Wednesday, June 21, 2017

MAFUNZO YA MAISHA YETU NI HAPA HAPA DUNIANI

Jamani ndugu zangu wapendwa, leo tarehe 21 june 2017 muda wa asubuhi nikiwa natoka nyumbani kuelekea Kazini nje ya geti machozi yaliyotoka kwa kile nilichokiona.

Siku zote mama watoto ndie unifungulia geti ili nitoke nje,  lakini leo niliamua kufungua mwenyewe.

Nilipofungua geti tu mara nikamuona jamaa mmoja akipita karibu na geti letu na kunitazama mara moja akarudisha uso wake mbele na kuendelea na safari yake.

Nilipigwa na mshangao kwa sekunde kadhaa, kumbukumbu zangu zikiniambia ninamfahamu huyo jamaa.
Yule jamaa alikuwa amebeba mfuko mkubwa ndani yake kuna chupa chakavu za plastiki au PET.

Ndugu yangu wee wacha tu. Kwa sauti kubwa nikamuita yule jamaa fulani fulani simama huku nikisema "ata kama upo katika mazingira magumu lakini mimi siwezi kuacha kukusalimia"

Akasimama na kurudi nyuma nilipo, kwa mshangao machozi  yakinitoka kidogo  dogo na simanzi ya huruma  inatawala juu yangu jinsi alivyo na mapito ya maisha anayopitia kwa sasa.

Najua bado unajiuliza maisha yake yalikuwa vipi na kwa nini machozi yanitoke.

Huyu kijana alikuwa akifanya kazi katika kampuni moja na nafasi nzuri ya kipato kizuri kwa mwezi.

Alikuwa akifanya biashara yake binafsi ya kupiga picha.

Alikuwa ni mwangaikaji katika kazi zake za kila siku.

Jirani mwema na mtanashati na mcheshi wa mienendo yake.

Angalia maisha yalivyo na kitendawili kwa binadamu.

Unayotenda leo ni yale utendayo sasa hapa duniani, na kesho ni siku yako mpya katika matendo yako utayoyatenda siku hiyo hapa hapa duniani.

Jifunze matendo mema kabla ujachelewa ili ujenge nafsi iliyo safi kwa imani uliyopewa na Mungu wetu.

Mwangalie huyu kijana jinsi alivyokuwa mwanzo na sasa jinsi maisha yake yavyoenda.

Ni tofauti na jana amekuwa kijana yule yule lakini tabia na mwelekeo umebadilika kabisa, toka mtanashati mpaka muokota chupa zilizotupwa mitaani.
Uchungu wa moyo wangu ndio kichocheo cha kuandika makala hii fupi.

Ndugu yangu Amini maisha ni fundisho tosha kwa wengine.

Na leo yako sio sawa na kesho yako.

Wako
Kennedy Kimaro
kimarokenny@gmail.com

Saturday, June 17, 2017

NJIA YA MTU MBAYA NI CHUKIZO KWA BWANA

Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake. 
Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali humpenda mtu afuatiaye wema. 

Friday, June 16, 2017

MIMI NIMEMWINIUA KATIKA HAKI

Mimi nimemwinua katika haki, nami nitazinyosha njia zake zote; ataujenga mji wangu, naye atawaacha huru watu wangu waliohamishwa, si kwa kulipwa fedha, wala kwa kupewa zawadi, asema Bwana wa majeshi.

Thursday, June 15, 2017

Maana Bwana, aliyeziumba mbingu, asema hivi;

Maana Bwana, aliyeziumba mbingu, asema hivi;
Yeye ni Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; ndiye aliyeifanya imara; hakuiumba ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu;
Mimi ni Bwana, wala hapana mwingine. 

Saturday, December 31, 2016

Heri ya mwaka 2017.

Hebu tazama safari ya maisha hapo mwanzo na sasa.

Pili jeuka upande wa pili uyatazame maisha ya jirani au washirika wenzako katika maisha yao ya kila siku.

Vuta picha ni vikwazo gani, au miangaiko gani unayopitia kila siku ya maisha yako.

Jitazame wewe kama wewe Mungu amekupa nini kama ufunguo wa maisha yako ya kila siku kama zawadi ya mafanikio.

Sasa angalia hiyo miezi kumi na mbili umefanya nini katika mzunguko wa miangaiko yako ya kila siku.

Tazama kwa marefu na mapana umetenda mema mangapi, hesabu na yatafakari kwa pande zote.

Bado ujachelewa tazama yote mabaya uliyotenda na sema kwa bwana Mungu kuwa yaliyopita yamepita mwambie akupe msamaha, muombe akupe nafasi uwe msafi na kutorudia tena makosa.

Hapo utakuwa umeuanza mwaka mpya 2017 ukiwa msafi na upo tayari kwa matendo mema.

KARIBU MWAKA 2017 MIMI KENNEDY LEPATA CALIST KIMARO NIKIWA NA JOYCE KENNEDY MAMA WATOTO PAMOJA NA WATOTO BERTHA KENNEDY, MARTHA KENNEDY, JONATHAN KENNEDY NA JANET KENNEDY  TUNAWATAKIA HERI YA MWAKA MPYA 2017.

Thursday, December 15, 2016

MAISHA YA LEO NA KESHO KWA KIJANA SEHEMU YA PILI

MSINGI WA KWANZA NI IMANI

IMANI NI MSINGI AMBAO UNAKUFANYA KUWA NA MATENDO YANAYOLETA TABIA NJEMA ILIYO NA UPENDO WA KWELI KATIKA MAISHA YAKO YA KILA SIKU.

IMANI INAKUFANYA UWE NA UTIIFU KWA MUNGU WAKO.

MUHIMU KWA KIJANA WA LEO NI KUJENGE UHUSIONO BORA KATI YA FAMILIA TOFAUTI.

NENO FAMILIA SIO UDUGU WA UZAO WAKO BALI MKUSANYIKO WA WATU MNAOISHI KWA IMANI KUPITIA MUNGU BABA ILI KUJENGA UPENDO WA KWELI

KIJANA SHUPAVU WA JINSIA YOYOTE LAZIMA USIMAME IMARA KATIKA IMANI NA UPANGAJI WA MAMBO YAKO UNAYOYAFANYA KILA SIKU.

KUMBUKA KIJANA  MWENYE KUTENDA MATENDO YENYE TABIA NJEMA NA MWENENDO WA HESHIMA  KWA KUMPENDA MUNGU NA JAMII ILIYOMZUNGUKA.

YEYE NDIYE KIONGOZI BORA KATIKA JAMII.

TABIA YA KIJANA SIO NYUMBANI TU UNAPOKUWA MASOMONI KAMA MWANAFUNZI NDIPO UNAJIFUNZA MAMBO MENGI YENYE TABIA ZA WATU TOFAUTI UWAPO SHULE AU CHUO.

KWANINI CHUO NA SHULENI

KWA SABABU SEHEMU AMBAYO HUYU KIJANA WA LEO KAMA MWANAFUNZI UWA ANAJIFUNZA TABIA ZILIZO NZURI AU ZENYE MAADILI YASIO FAA KWA JAMII KUTOKANA NA KUWEPO KWA VIJANA TOFAUTI TOKA MAKAZI TOFAUTI.

MARA NYINGI SHULENI AU CHUO UWA PANA CHANGAMOTO KWA KIJANA KUWA NA MSIMAMO WENYE MANUFAA ILI BAADAE ASIMAME YEYE MWENYEWE

WAKATI MWINGINE VIJANA WANAJIKITA KATIKA MATENDO MABAYA  KAMA
UTUMIAAJI WA MADAWA YA KULEVYA NA MAMBO YASIYO KUBALIWA NA JAMII KWA UJUMLA.

SHULE NYINGI UWA ZINAWAJENGA VIJANA KATIKA MISINGI YA KUSIMAMA WAO WENYEWE ILI WAWEZE KUJITEGEMEA KUTOKANA NA MASOMO WANAYOWAFUNDISHA.

VIJANA LEO WANA CHEPUKA KATIKA MASOMO YA AINA TOFAUTI ILI BAADAYE WAWE WATU MUHIMU KATIKA JAMII KAMA

WAANDISI AU WANASAYANSI AU MADAKTARI AU WAHASIBU NA VIONGOZI KATIKA SEKTA TOFAUTI ZA JAMII.

Itaendelea
Kennedy Kimaro

KIJANA WA LEO BAADA YA KUMALIZA CHUO AU SHULE.

HAPA NDIPO MAJARIBU YA MAISHA NA KITENDAWILI CHA MAISHA KINAPONZIA

MARA NYINGI MTAZAMO WA MAISHA INATEGEMEA UNATOKEA FAMILIA GANI 

KAMA UNATOKA FAMILIA YENYE UWEZO KIDOGO NI NAFUU KATIKA KUINGIA MAISHA YA KIJANA WA LEO

KAMA UNATOKA KATIKA FAMILIA MASIKINI  HAPO CHANGAMOTO ZA KUANZA MAISHA NI NGUMU 

NYAKATI NYINGINE HUYU KIJANA WA LEO ANACHOKA NA KUJIKITA KATIKA MIENENDO MIBAYA YENYE KUTISHA KWA KIJANA WA LEO.

KATIKA NCHI ZINAZOENDELEA ZINAONESHA VIJANA WENGI HAWANA KAZI 

HEBU TUANGALIE KATIKA GOOGLE SEARCH TUONE WANASEMAJE SUALA LA AJIRA KWA VIJANA WA AFRIKA.

"Ukosefu wa ajira ni tatizo la ujumla katika Afrika, kinachotakiwa ni lazima kuwe ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi ili kulishughulikia. ... Kwa mujibu wa takwimu kutoka Shirika la Kazi Duniani (ILO) katika Afrika kusini mwa Sahara, vijana wenye ukosefu wa ajira wanafikia karibu asilimia12 kutokana na takwimu za .Apr 1, 2016

NAFIKIRI UMEFUNGUA MAWAZO KIDOGO KUJUA KIJANA WA LEO ANAVYO ELEKEA KUWA NA MAJUKUMU MAGUMU 

AJIRA INAVYO KUWA TATA KATIKA AFRIKA KWA UJUMLA KWA KIJANA WA LEO.

Itaendelea

KENNEDY KIMARO

16-12-2016

AJIRA INAPOKUWA NGUMU KWA KIJANA WA LEO

KWANZA KIJANA MWENYE MISINGI BORA YA IMANI UWA HAKATI TAMAA KATIKA MIANGAIKO YAKE YA KUTAFUTA KAZI

HICHO KINAKUWA KIPINDI CHA MAPITO KWA KIJANA WA LEO.

MARA NYINGI HUYIU KIJANA WA LEO UWA ANAPATA MAJARIBU MENGI.

WAKATI WA KUTAFUTA KAZI UTAPITA KILA KONA YA MJI NA UTASOMA HABARI ZA KUTATAFUTA NAFASI ZA KAZI KWA NGUVU ZAKO ILI MAISHA YAENDELEE.

WAKATI WA MIANGAIKO NA BAADA YA KUFANYA INTERVIEW MAENEO TAFAUTI BILA KUCHOKA.

KILA UENDAKO KWENYE INTERVIEW UTAKUTANA NA SWALI MOJA LENYE KUMCHOSHA MAWAZO KIJANA WA LEO.

SWALI LENYE NI HILI

Je unao uzoefu wa miaka mingapi kazini. 

Wakati huyu kijana wa leo, ndio katoka chuo au shule miezi kazaa iliyopita.

JIBU TOKA KWA KIJANA WA LEO NI HILI HAPA CHINI.

Nilipokuwa chuo nilikuwa nikifanya mazoezi ya kikazi sehemu inayoendana na masomo yangu.

Uzoefu wangu ni elimu yangu na nilichokisema hapo mwanzo. 

WAKATI KIJANA WA LEO ANAPOKUWA AKISUBIRI MAJIBU YA MAJARIBIO YA KAZI 

NDIPO WANAPOJITOKEZA WATU WA KATI AU VIJANA WA MJINI NA KUSEMA WANAWEZA KUMSAIDIA KUPATA AJIRA.

HUYI KIJANA WA MJINI NI MTU WA AINA GANI. 

NI MTU WA KATI KAZI YAKE NI KUPATA FEDHA BILA KUWAJIBIKA AU UTAPELI KWA JINA LA MJINI.

HAPA KIJANA ANAKUWA NJIA PANDA 

INAYOWEZA KUMTAMANISHA KUWA KIJANA WA MJINI 

AU KUVUTA SUBIRA ILI APATE AJIRA ILI MAISHA YAENDELEE KWA AMANI YENYE UPENDO WA KWELI.

MARA NYINGINE UWEZO WAKE WA ELIMU NI CHACHU TOKA KWA VIJANA WA MJINI WA KUTAKA KUMTUMIA KAMA MTU WA KATI KWA KAZI NYINGINENE ZENYE KUITAJI MSOMI.

IMANI NDIYO MSINGI WA KUTOJIINGIZA KATIKA KAZI ZISIZO FAIDA NA DHAMANA KWA JAMII.

Itaendelea 

Kennedy KimaroZ 

18/December/2016


KIJANA ANAYETOKA FAMILIA YENYE UWEZO YUPO KAZINI ILI MAISHA YAENDELEE.

MARA NYINGI VIJANA TOKA FAMILIA ZENYE UWEZO WANAYO BAHATI YA KUPATA AJIRA MAPEMA KUTOKANA NA UWEZO WA ELIMU ZAO TENA WANAPATA AJIRA KATIKA MAKAMPUNI BINAFSI AU IDARA ZENYE KUESHIMIKA KATIKA JAMII KUTOKANA NA NGUVU YA FAMILIA ZAO.

HUYU KIJANA ANAPOANZA KAZI ANAFANYA KAZI KWA BIDII NA UWEZO WAKE WOTE KATIKA KIPINDI CHA UANGALIZI ANAKUWA MWAMINIFU NA KUKIZI MATAKWA YANAYO SABABISHA KUPEWA AJIRA YA KUDUMU.

LAKINI KUTOKANA NA IMANI DUNI NA USHAWISHI WA KIDUNIA KIJANA MWENYE FIKRA YA  KUTAKA UTAJIRI WA HARAKA ANABADILIKA KUWA NA SURA YA RUSHWA NA UFISADI.

KIJANA TOKA FAMILIA YENYE UWEZO ANAPOKUWA MZOEFU KAZINI KWA KUJUA NJIA ZA MKATO MARA NYINGI MSHAHARA WAKE SIO BAJETI YAKE YA MATUMIZI BALI PESA ANAYOIPATA KWA RUSHWA PEMBENI NDIO MSHAHARA WAKE WA MATUMIZI.

HUYU KIJANA WA LEO MWENYE MWELEKEO WA TAMAA YA UTAJIRI WA KIFEDHA NA KUWEKEZA MITAJI MIKUBWA KAMA WANAVYOMILIKI FAMILIA YAKE KIJANA ANAKUWA NJIA PANDA AMBAYO.

INASABABISHA NYAKATI NYINGINE KUJIKITA KATIKA MAMBO TOFAUTI YANAYOMSHAWISHI KUFANYA VITU KINYUME NA UTARATIBU WA SHERIA ANAFANYA VITU VINAVYO PIGWA VITA KATIKA JAMII KAMA.

RUSHWA UPENDELEO KWA WATU WASIOSTAILI NA KUWANYIMA HAKI WANAOSTAILI ILI KUMPATIA NGUVU YA KUPATA PESA KWA NJIA ZISIZO SAHIHI.

KUJIINGIZA KATIKA MAISHA YENYE UHUSIANO WA RUSHWA NA UNYANYASAJI KWA WENGINE  KUPITIA MADARAKA YAKE ALIYOPEWA KUSAIDIA JAMII NA TAIFA LAKE.

VIJANA WENGI WA JAMII HII UFUKUZWA AU KUSIMAMISHWA KAZI KUTOKANA NA FIKRA ZAO ZA UTAJIRI WA HARAKA KATIKA MAWAZO YAO.

LAKINI KWA UPANDE MWINGINE VIJANA WENGINE TOKA FAMILIA ZENYE UWEZO WANAKUWA NA UWEZO MKUBWA KATIKA UTENDAJI NA KUTOA MSAADA KWA JAMII NA TAIFA KWA UJUMLA.

MARA NYINGI UNAKUTA VIJANA WANAOTOKEA KATIKA FAMILIA ZENYE UWEZO HAWANA TAMAA NDOGO NDOGO KATIKA KUPOKEA RUSHWA YA FEDHA AU UNYANYASAJI NA UBINAFSI KATIKA KAZI ZA JAMII 

UTAKUTA VIJANA HAWA WAMEBOBEA KATIKA MSINGI WA IMANI UNAWOWAJENGA KUWA NGUVU NA UWEZO WA KUFANYA KAZI KATIKA JAMII NA TAIFA LAKE.

FAMILIA ZENYE UWEZO ZINAPENDA KUWEKEZA KATIKA IMANI ILI FAMILIA IWE NA MSINGI WENYE KUESHIMIKA KATIKA JAMII NA TAIFA.

HAPO KIJANA WA LEO ANAPOKUWA NA MWELEKEO WA WAZAZI KATIKA IMANI BASI YEYE UWA NA NGUVU ULIYO MSAADA WA MWENYEZI MUNGU KATIKA KUSIMAMA KWENYE IMANI YA KWELI ILI KUIJENGA JAMII ILIYO BORA.

NDIO MAANA VIJANA WOTE WALIO. KATIKA MSIMAMO WA KIMUNGU BASI IMANI YAO INAWAPA NGUVU YA KUFANYA YALIYO MEMA NA YANAYOKUBALIKA KATIKA KIJAMII NA TAIFA KWA UJUMLA.

Itaendelea 

Kennedy Kimaro 

26/December/2016

Wewe kama kajana wa leo simama na imani uliyopo sasa, au badilika na ufuate kile nafsi yako inavyokutuma kwa wakati uliopo sasa.

Kumbuka nafsi yako ni lazima ijengwe katika imani inayomwamini muumba wa mbingu na vitu vinavyoonekana na visivyoonekana.

Kataa kabisa na kamwe usifanye nafsi yako iwe nafsi ya mwenzako, kamwe kataa nguvu za kishetani kukuongoza katika imani potofu.

Kumbuka kila ufanyacho wewe, kitabaki kuwa chako na kitakupa sifa ya matendo yako wewe binafsi. 

Yawe mabaya au mazuri ni yako wewe binafsi daima milele.

Na hakuna atayepunguza au kuongeza lolote kwako, kwani wewe umepewa roho yenye kuwakilisha uhai wako hapa duniani.

Mwache yeye ajenge matendo yake kama yeye binafsi.

Kwani na yeye anapaswa kukuachia wewe ujenge yako yaliyo mema kwa ramani ya maisha yako kwa kutumia viongozi wateule wa Mungu.

KIJANA WA LEO TAZAMA MBELE KWA NGUVU YA IMANI ILI IKUSAIDIE KUSIMAMA IMARA MUDA WOTE.

NARUDIA TENA KUSEMA HILI 

HAPO ULIPO SASA NDIPO ULIPO WEWE MWENYEWE KAMA NAFSI YAKO INAVYOKUTUMA KUFANYA KITU CHOCHOTE. 

BASI IPE NAFSI YAKO NGUVU YA MUNGU IKUTUME KAMA WEWE NA IMANI YAKO MWENYEWE.

KILA KITU UNACHOAMUA BASI KIWE CHA IMANI AMANI NA UPENDO WA KWELI NDANI YAKE.

NARUDIA TENA SIKU ZOTE CHELEWA KUAMUA KITU CHENYE UTATA KWA KUNYAMAZA KIMYA 

PILI SIKILIZA WENGINE WANASEMAJE 

TATU CHANGANYA NA YAKO ILI UPATE LILILO JEMA NA LENYE UPENDO WA IMANI NA AMANI NDANI YAKE. 

TAMBUA SIFA YA IMANI YAKO IPO KWAKO NA KWA MUNGU NDIO MAANA WEWE UNAJUA YAKO YALIO KATIKA MAWAZO YAKO

LAKINI MUNGU TAYARI ANAJUA KILA LILILO KATIKA MAWAZO YAKO KABLA WEWE UJAWAZA 

INAMAANA MUNGU ANAJUA KILA KITU JUU YAKO.

UJACHELEWA KIJANA WA LEO TAZAMA MBELE MAISHA YA KWA IMANI MOJA TU NAYO NI MUNGU AMBAYE YUPO LEO NA MILELE DAIMA.

Itaendelea 

Kennedy Kimaro 

28/12/2016




Tuesday, December 13, 2016

MAISHA YA LEO NA KESHO KWA KIJANA WA LEO

UKINIONA NATABASAMU KWA MBALI HUKU  NACHEKA CHINI CHINI

NAJUA UTANIULIZA KWANINI NINAFANYA HIVYO

JIBU LAKE NAKUMBUKA MSEMO WA ZAMANI ULIKUWA UNASEMA HIVI

KUWA MWANANGU UYAONE YA DUNIA

NAJUA BADO UNAJIULIZA KWA NINI NAYASEMA HAYO.

BASI TWENDE NA MIMI UTAJUA KWA NINI NILISEMA "KUWA MWANANGU UYAONE DUNIA"

DUNIA YENYEWE IPO SAFARINI AMBAYO ISIYO NA MWISHO ILA KILA KIUMBE KINA MWISHO

KAWAIDA DUNIA INALIZUNGUKA JUA PIA INAJIZUNGUSHA YENYEWE KATIKA MUHIMILI WAKE.

CHA AJABU NJIA UNAYOPITIA DUNIA TOFAUTI KILA WAKATI KWA MAHESABU YA MUUMBA MWENYEWE

TENA AMEVIPANGA VITU VINAVYO FANANA NA DUNIA KATIKA ANGA ZA JUU NA PIA VINALIZUNGUKA JUA KWA MAHESABU YA AJABU NA TECHNOLOJIA ISIYO NA MFANO WAKE

HAPO NDIO UNAPATA KITU KINACHOITWA MAISHA YANAYOPATIKANA KWA KILA KIUMBE KILICHO NDANI YA DUNIA HII TUNAYOISHI SASA

KATIKA MAISHA UTAPATA KITU KINACHOITWA LEO NA KESHO UKIFANYA MAHESABU UTAPATA LEO NA KESHO

JIBU LAKE MAISHA YALIPO ANZA TANGU  UKIWA TUMBONI KWA MAMA YAKO MPAKA KUZALIWA KWAKO HAPA DUNIANI NA MAISHA YA YA LEO

AU WEWE UNASEMA JUU YA LEO NA KESHO.

HEBU TWENDE NA MIMI ILI TUJUE  MTAZAMO WA MAWAZO YANGU YAMESIMAMA WAPI KWENYE HIYO LEO NA KESHO.

NAREJEA KUSEMA YOTE NI YANGU NI SIO KWA MTU MWINGINE KWANI YEYE ANAO MTAZAMO WAKE.

TUANZE NA LEO

TAZAMA LEO KAMA KIJANA ALIYEKUWA NA KUTIMIZA MIAKA 18 ITAKAYOKUPA NGUVU YA KUFANYA MAMBO YAKO KAMA YEYE KIJANA WA LEO

TAZAMA PALE MZAZI ANAPOKUWA NA WASIWASI WA MATENDO UNAYOTENDA KILA SIKU AMBAYO KWA MTAZAMO WANGU NDIYO NYAKATI ZA LEO KWA KIJANA

EBU TAZAMA VINGAPI UNAVIFANYA KWA HESHIMA ZA PANDE ZOTE KATIKA FAMILIA YAKO.

KUMBUKA WEWE BADO UPO CHINI YA WAZAZI KWA UPANDE MMOJA NA UPANDE MWINGINE UNAWAZA KUJENGA MWELEKEO WAKO KAMA KIJANA LEO

SASA KAZI INAKUJA PALE WAZAZI WAKO ALIPOKUWA UNAISHI NA WAZAZI WAKO WALIKUPA MAFUNDISHO YA IMANI NA KIDUNIA ILI KUISHI KATIKA DUNIA YENYE TABIA TOFAUTI

TENA WATU WANAKUANGALIA UWEZO WAKO WA IMANI NA ELIMU YA KIDUNIA UMESIMAMA UPANDE GANI.

MARA NYINGI MISINGI HIYO MIWILI NDIO ITAKUPA MWELEKEO WAKO KATIKA NYAKATI ZA LEO.

Tutaendelea
KENNEDY KIMARO

MSINGI WA KWANZA NI IMANI

IMANI NI MSINGI AMBAO UNAKUFANYA KUWA NA MATENDO YANAYOLETA TABIA NJEMA ILIYO NA UPENDO WA KWELI KATIKA MAISHA YAKO YA KILA SIKU.

IMANI INAKUFANYA UWE NA UTIIFU KWA MUNGU WAKO.

MUHIMU KWA KIJANA WA LEO NI KUJENGE UHUSIONO BORA KATI YA FAMILIA TOFAUTI.

NENO FAMILIA SIO UDUGU WA UZAO WAKO BALI MKUSANYIKO WA WATU MNAOISHI KWA IMANI KUPITIA MUNGU BABA ILI KUJENGA UPENDO WA KWELI

KIJANA SHUPAVU WA JINSIA YOYOTE LAZIMA USIMAME IMARA KATIKA IMANI NA UPANGAJI WA MAMBO YAKO UNAYOYAFANYA KILA SIKU.

KUMBUKA KIJANA  MWENYE KUTENDA MATENDO YENYE TABIA NJEMA NA MWENENDO WA HESHIMA  KWA KUMPENDA MUNGU NA JAMII ILIYOMZUNGUKA.

YEYE NDIYE KIONGOZI BORA KATIKA JAMII.

TABIA YA KIJANA SIO NYUMBANI TU UNAPOKUWA MASOMONI KAMA MWANAFUNZI NDIPO UNAJIFUNZA MAMBO MENGI YENYE TABIA ZA WATU TOFAUTI UWAPO SHULE AU CHUO.

KWANINI CHUO NA SHULENI

KWA SABABU SEHEMU AMBAYO HUYU KIJANA WA LEO KAMA MWANAFUNZI UWA ANAJIFUNZA TABIA ZILIZO NZURI AU ZENYE MAADILI YASIO FAA KWA JAMII KUTOKANA NA KUWEPO KWA VIJANA TOFAUTI TOKA MAKAZI TOFAUTI.

MARA NYINGI SHULENI AU CHUO UWA PANA CHANGAMOTO KWA KIJANA KUWA NA MSIMAMO WENYE MANUFAA ILI BAADAE ASIMAME YEYE MWENYEWE

WAKATI MWINGINE VIJANA WANAJIKITA KATIKA MATENDO MABAYA  KAMA
UTUMIAAJI WA MADAWA YA KULEVYA NA MAMBO YASIYO KUBALIWA NA JAMII KWA UJUMLA.

SHULE NYINGI UWA ZINAWAJENGA VIJANA KATIKA MISINGI YA KUSIMAMA WAO WENYEWE ILI WAWEZE KUJITEGEMEA KUTOKANA NA MASOMO WANAYOWAFUNDISHA.

VIJANA LEO WANA CHEPUKA KATIKA MASOMO YA AINA TOFAUTI ILI BAADAYE WAWE WATU MUHIMU KATIKA JAMII KAMA

WAANDISI AU WANASAYANSI AU MADAKTARI AU WAHASIBU NA VIONGOZI KATIKA SEKTA TOFAUTI ZA JAMII.

Itaendelea
Kennedy Kimaro

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.comme google-site-verification=Qm-XNfnL5kai8WV2inT1RRX2WIPaBTG_WPq3kYSBwbgKennedy Kimaro 2008 NYUMBANI NI NYUMBANI TU KUMBUKA KUWEKEZA NYUMBANI LEO

Rudi TOP-Juu