Wednesday, July 4, 2007

Mwandishi wa BBC Gaza aachiliwa





.


Allan Johstone baada ya kuachiliwa
Sikiliza Dira ya DuniaMwandishi wa BBC katika Gaza, Alan Johnston, aliyeachiliwa usiku wa kuamkia leo baada ya takriban miezi minne ameshukuru juhudi za Kimataifa za kutaka aachiliwe.
Akizungumza kwa njia ya simu na wenzake wa BBC kutoka Ubalozi wa Uingereza mjini Jerusalem baada ya kuondoka GAZA, Bw Johnston amesema kuwa kwa bahati aliweza kuipata Redio na hivyo kuweza kufuatilia jitihada zilizokua zikifanywa kutaka aachiliwe, jambo ambalo lilimpa matumaini.
Hapo awali, akionekana mwenye afya nzuri ingawa mchovu , alielezea majuma kumi na sita ya kuzuiliwa kwake katika chumba kifinyu kama kuzikwa mzima.
Na wazazi wa Alan wameelezea idhaa ya Kiswahili ya BBC kwamba wamepata faraja kubwa isiyoelezeka kufuatia kuachiliwa kwake.
Babake Alan Bwana Graham Johnstone amesema asingependa mwanawe kurudi mashariki ya kati.

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.comme google-site-verification=Qm-XNfnL5kai8WV2inT1RRX2WIPaBTG_WPq3kYSBwbgKennedy Kimaro 2008 NYUMBANI NI NYUMBANI TU KUMBUKA KUWEKEZA NYUMBANI LEO

Rudi TOP-Juu