Saturday, November 24, 2007

Mwacheni Zitto Kabwe afanye kazi












Mwacheni Zitto Kabwe afanye kazi
Na Gladness Mboma


HII inashangaza pale ambapo baadhi ya viongozi wa Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) wanapompinga mwenzao, ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini Bw. Zitto Kabwe kuteuliwa na Rais Jakaya Kikwete katika Kamati ya Taifa kuangalia mustakabali wa Taifa wa rasilimali ya madini. Hivi karibuni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete ameunda Kamati ya Kuangalia Upya Mikataba ya Uchimbaji Madini Nchini kwa kuwateua Mwenyekiti na wajumbe 11 watakaofanya kazi kwa kipindi cha miezi mitatu. Kamati hiyo inashirikisha wanasiasa kutoka chama tawala na wale wa upinzani wakiwemo wadau kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali na wataalam kutoka sekta mbalimbali Moja ya mambo yaliyosababisha majadiliano na mabishano makali ndani ya CHADEMA ni uteuzi wa kamati au tume hiyo ya kutazamia upya mikataba ya madini iliyowekwa kati ya wawekezaji na Serikali iliyoteuliwa na Rais Kikwete. Rais Kikwete aliweka wazi suala la kuundwa tume hiyo wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) uliomalizika hivi karibuni mkoani Dodoma. Katika mkutano huo Rais Kiwete alitoa ahadi hiyo baada ya matukio mengi ya kukashifiana baina ya viongozi wa Serikali na baadhi ya vyama vya upinzania hasa ujulikanao kama Muungano wa Vyama vinne vya Upinzania. Malumbano hayo ya kukashifiana yalikuwa yamezidi katika upande wa vyama vya upinzania, yakidai kuwa Serikali ilikuwa haifaidiki na rasilimali yake. Kutokana na kuruhusu mikataba ya uchimbaji madini hapa nchini iliyowapendelea zaidi wawekezaji na Taifa kuambulia faida ndogo na kusababisha hasara. Kashfa hiyo ilipamba moto hasa baada ya watendaji wa Serikali kwa maana ya mawaziri na viongozi wengine wa ngazi za juu katika taasisi muhimu na nyeti kutajwa hadharani kuhusika na vitendo vya rushwa. Zaidi ya jambo lililofumua malumbano na kashfa hizi ni sakata la mikataba ya madini na hasa mkataba wa madini wa Buzwagi ambao Waziri wa Nishati na Madini Bw. Nazir Karamagi kudaiwa kuusaini akiwa nje ya nchi na kwamba haukuwa na maslahi kwa Serikali. Aliyeibua hoja hiyo hakuwa mwingine bali ni Bw. Kabwe ambaye aliyatoa wazi bungeni na kumletea matatizo yaliyosababishia kusimamishwa na kutojishughulisha na shughuli zozote za Bunge, adhabu ambayo kwa sasa imemalizika. Baada ya kusimamishwa kwa Bw. Kabwe, vyama hivyo vinne vya upinzani vilianza kuzunguka nchini kuelezea umma wananchi kuhusiana na mkataba huo, na kuelekeza shutuma mbalimbali serikalini. Ni kweli vyama hivyo viliweza kuwateka wananchi kutokana na jinsi walivyokuwa wakieleza na kutoa vielelezo mbalimbali vilivyosababisha baadhi ya wananchi kuamini, walichokuwa wakisema. Baada ya malumbano hayo ya muda mrefu Rais Kikwete bila hiana aliunda tume ambayo imewashirikisha pia viongozi wawili wa vyama vya upinzani. Tume hiyo ambayo ni watu makini iliwafurahisha Watanzania wengi na watu kufurahia uteuzi huo ambao ni wa kidhati uliofanywa na Rais wetu makini na kuzidi kumuongezea heshima. Kilichowafurahisha zaidi Watanzania ni pale Rais Kikwete alipoteua pia viongozi kutoka vyama vya upinzania na hasa ukizingatia kuwa wapinzani hao ni kati ya wasemaji wazuri katika vyama vyao. Lakini pamoja na uteuzi huo kinachoshangaza ni kwamba baadhi ya wapinzani hao hao waliotaka kuundwa kwa tume ya aina hiyo wanataka kukwepa majukumu yao kama Watanzania, sasa wanataka Bw. Kabwe ajitoe kwa maelezo kuwa akiingia katika kamati hiyo atazibwa mdomo. Bw. Kabwe ninayemfahamu mimi na anayefahamika kwa Watanzania wote kutokana na ukakamavu wake na mwenye uchungu na nchi yake kamwe hawezi kuzibwa mdomo kama wasemavyo baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani kikiwemo chama chake. Malumbano hayo hayalengi kulinufaisha Taifa, bali ni kuleta mgawanyiko ndani ya Taifa. ============ Upinzani wa kisiasa unatakiwa kuimarisha demokrasia na kuchochea maendeleo katika nchi husika, iweje leo hii Rais anateua mmoja wapo katika kambi hiyo ili aweze kutoa mchango wake kwa manufaa ya Taifa anazuiwa? ============= Sasa vyama vya upinzani mnakoelekea ni kubaya inaelekea nchi hii amuitakii mema, ni kwa nini mnapingana na yale ambayo yamefanywa na Rais wetu kwa manufaa ya nchi? Je, Rais asingeteua tume hiyo mpaka sasa mngekuwa mmezusha jambo gani, tufike mahali sasa tusiwe vyama vya upinzani vya kuleta fujo, Watanzania hawafurahishwi na uamuzi mnaofanya. Inasikitisha kuona baadhi ya watu tunaowategemea kuwa wamekomaa kisiasa wanataka kurudisha nyuma maendeleo ya nchi na kuanzisha malumbano yasiyokuwa na faida kwa Watanzania. Nilitegemea baada ya Rais kumteua Bw. Kabwe mngemwombea ili aweze kuifanya kazi yake vema badala yake mnamkatisha tamaa kana kwamba alichofanya Rais Kikwete ni kunyume. Kinachotakiwa ni kuiachia tume hiyo ya watu makini kufanya kazi yake kwa umakini tupate kujua kilichotokea na aliyesababisha ni nani na si vinginevyo, kwani hatutafika popote tukiendekeza malumbano.


Uchunguzi dhidi ya mtoto wa Rais Karume wapelekwa serikalini

Na Tausi Ally
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam, imekamilisha uchunguzi dhidi ya tuhuma zinazomkabili Wakili wa Kujitegemea, Fatuma Karume na kupelekwa uongozi wa juu serikalini.
Fatuma ambaye ni mtoto wa Rais wa Zanzibar, Aman Karume anadaiwa kumtolea maneno makali Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo, Addy Lyamuya.
Akizungumza ofisini kwake jana, Hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi, Sivangilwa Mwangesi alisema tayari taarifa hizo zimetumwa uongozi wa juu wa serikali kwa ajili ya kufanyiwa kazi.
Hakimu Mwangesi alisema kuwa, baada ya uchunguzi kufanyika, imebainika kuwa wakili huyo alifanya fujo mahakamani.
� Kwa maoni yangu na maelezo ya mashahidi walioshuhudia tukio, wamebaini kuwa ni kweli Karume alifanya fujo mahakamani, � alisema Hakimu Mwangesi.
Hakimu Mwangesi, alisema Hakimu Lyamuya hakuweza kumchukulia hatua wakili huyo, kwa madai kuwa, alipigwa na butwaa kutokana na kutoamini wala kutegemea kama wakili huyo angemtolea maneno makali na ya vitisho.
Alisema taarifa kwamba Hakimu Adolf Mahay anahusika na tuhuma za rushwa kama inavyodaiwa na Karume ni za uongo na kwamba hajapokea maelekezo yoyote kutoka ngazi ya juu serikalini za kumsimamisha kazi hakimu huyo.
Naye Hakimu Mahay alipohojiwa kuhusiana na tuhuma hizo, alisema hawezi kuongea chochote kwa kuwa si mwanasiasa na kwamba angekuwa amehusika na rushwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), wangemkamata na kumchukulia hatua za kisheria.
�Na hili la Kisutu kuwa inanuka rushwa ni maoni yao wenyewe walioandika, ninachojua mimi Kisutu ni nzuri na inapinga rushwa,� alidai Hakimu Mwangesi.
Kuhusu kesi hiyo kupangwa kwa hakimu mwingine, Mwangesi alisema hivi anatafuta ushauri kwa kuwa mtoto huyo wa Karume, alisema kuwa mahakimu wote wanakula rushwa.
Alisema pia anasubiri barua ya Karume endapo ataandika kuondoa kesi hiyo katika mahakama hiyo au la kwani Novemba 21, mwaka huu wakati amkipelekea malalamiko dhidi ya Hakimu Lyamuya, alimwambia kwamba ataiondoa.
Novemba 22, mwaka huu, Hakimu Lyamuya aliwasilisha malalamiko Chama cha Wanasheria Tanzania (TLS) dhidi ya wakili huyo wa kujitegemea akimlalamikia kwa kumfokea mahakamani na kumtolea lugha ya vitisho.
Taarifa za kupokewa kwa malalamiko hayo TLS zilithibitishwa na Rais wa Chama hicho, Joaquin ambaye alisiditiza chama kinajukumu la kumtetea au kumuadhibu mwanachama endapo atabainika kukiuka maadili ya taaluma hiyo.

Friday, November 23, 2007

Tiba MOI:Aliyepasuliwa mguu badala ya kichwa, afariki










Tiba MOI:Aliyepasuliwa mguu badala ya kichwa, afariki

Jackson Odoyo na Andrew Msechu


EMMANUEL Mgaya (19), aliyefanyiwa upasuaji wa kichwa Jumatatu wiki hii baada awali kufanyiwa wa mguu kimakosa, katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI), amefariki dunia jana asubuhi.
Mara baada ya Mgaya kufanyiwa upasuaji wa kichwa, hali yake ilibadilika na kuwa mbaya kisha kulazwa chumba cha wagonjwa mahututi (ICU), hadi mauti yalipomfika jana saa 2:30 asubuhi.
Awali Mgaya alifanyiwa upasuaji wa mguu badala ya kichwa na Emmanuel Didas ya kichwa badala ya mguu, Novemba mosi mwaka huu katika taasisi hiyo.
Akizunguza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu muda mfupi baada ya Mgaya kufariki dunia, mmoja wa wauguzi wa MOI, alisema hali ya mgonjwa huyo, ilianza kuwa mbaya juzi mchana.
Alisema jana asubuhi mapema alipofika kazini, alimkuta akipumua kwa shida, hali iliyoonyesha alikuwa amezidiwa.
Aliongeza kuwa, baadaye madaktari wanaomuhudumia waliwasili katika chumba hicho na kugungua hali yake ilikuwa ni mbaya zaidi.
Hali ya mgonjwa huyo ilianza kuwa mbaya tangu jana (Juzi)mchana na niliporudi kazini leo (jana)alfajiri nilikuta hali yake imebadilika kiasi cha kunipa wasiwasi, lakini madaktari walifika muda mfupi badaye na kumpa huduma za haraka japo hazikuweza kumsaidia, � alisema muuguzi huyo ambaye hakupenda jina lake litajwe gazetini kwa kuwa si msemaji.
Kwa mujibu wa chanzo, jitihada za kuokoa maisha ya Mgaya zilishindika majira ya saa 2:30 mgonjwa huyo alifariki dunia.
Hata baadhi ya madaktari waliozungumza na Mwananchi walithibitisha kwamba Mgaya amefariki dunia.
�Kifo cha Mgaya kimetushutua sana kwa sababu tangu alipofanyiwa upasuaji wa mara ya kwanza kila daktari wa taasisi hii alijaaribu kumsaidia kwa karibu, � alisema daktari huyo.
Waliongeza kwamba hata Mkurugenzi Mkuu wa MOI, Profesa Laurent Museru, amesikitishwa sana na kifo hicho na kulazimika kuitisha kikao cha dharura kujadili namna ya kufikisha taarifa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii na kwa ndugu wa marehemu huyo.
Akizungumza na Mwananchi, Profesa Museru amethibitisha kutokea kwa kifo cha Mgaya.
�Ni kweli Mgaya alifariki dunia leo (jana) asubuhi na tumeshawajulisha ndugu zake pamoja kutoa taarifa wizarani, pia mwili wa marehemu umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti,alisema Profesa Museru.
Alisema kwamba utaratibu wa maziko yake, utafahamika baada ya kuwasiliana na ndugu zake. Mgaya ni mwenyeji wa Mkoa wa Iringa.
Habari za kifo cha Mgaya, si tu zimewashtusha wafanyakazi wa MOI, pia Waziri wa Afya, kimesema chanzo chetu cha habari.
Mgaya alifikishwa katika taasisi hiyo, Oktoba 28, mwaka huu akitokea mkoani Iringa na kufanyiwa uchunguzi wa kina kuhusu matatizo yake na madaktari kushauri afanyiwe upasuaji wa kichwa.
Mwanzoni mwa mwezi huu, badala ya kufanyiwa upasuaji wa kichwa, alifanyiwa upasuaji wa mguu, huku Didas akifanyiwa wa kichwa badala ya mguu.
Kwa sasa Didas amelazwa ICU katika taasisi hiyo huku kukiwa na habari kwamba amepoza upande wa kulia wa mwili.
Tokea Didas amefanyiwa upasuaji huo tata, hajaamka, wala hajaongea na kadri siku zinavyokwenda hali yake, inazidi kuwa mbaya.
Baada ya tukio hilo, Prof Museru aliamriwa na Bodi ya MOI, kuunda tume ya kuchunguza upasuaji huo na kutekeleza hilo, Novemba 2 mwaka huu.
Tume ilikamilisha kazi yake Novemba 13, na kuikabidhi Bod Novemba 15, na Bodi kuipeleka kwa Waziri Novemba 16.
Katika hatua nyingine, Waziri Mwakyusa ameahidi kutoa taarifa ya Tume hiyo iliyoundwa kuchunguza sakata la upasuaji huo.
Taarifa iliyopatikana jana kutoka katika wizara yake, ilifahamisha kuwa, Profesa Mwakyusa anatarajiwa kutoa taarifa hiyo leo saa 4.00 wizarani hapo.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi vifaa vya upimaji kwa ajili ya wagonjwa wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF) jijini Dar es Salaam jana, Mwakyusa aliahidi kutoa taarifa hiyo leo, baada ya kumalizia maandalizi ya mwisho.
Naombeni munivumilie kwa leo, ninamalizia utaratibu wa kuitoa, ila nitaitoa kesho , siewezi kuzungumza lolote leo kwa kuwa ninaweza kuzungumza nusu nusu, nivumilieni kama mlivyonivumilia tangu nilipowaomba kufanya hivyo nilivyokuwa Bungeni Dodoma, � Waziri huyo aliwaambia wanahabari waliotaka kujua hatma ya taarifa hiyo.
Alisisitiza kuwa, subira ni suala la msingi, hivyo wanachi hawana budi kusubiri kwa muda ili waweze kupata taarifa iliyokamilika.
Awali Prof Mwakyusa, alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari, akisema taarifa hiyo angeitoa juzi, lakini kwa sababu zisizojulikana, alishindwa kufanya hivyo.

Dk. Rashid aombwa arejee Tanesco



Waandishi WetuHabariLeo; Friday,November 23, 2007 @00:04
BODI ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania inambembeleza aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Dk. Idris Rashid aliyejiuzulu juzi, atengue uamuzi wake, imefahamika. Ingawa mamlaka zinazohusika hazikutaka kusema lolote kuhusiana na suala hilo lakini chanzo chetu cha habari kimethibitisha kuwa bado inamsihi Dk. Rashid abadili uamuzi wake. "Ni kweli tuko katika jitihada hizo za kuzungumza naye kuona kama atabadilisha uamuzi wake," alisema mjumbe mmoja wa bodi ambaye hakutaka jina lake litajwe gazetini. Dk. Rashid mwenyewe alipoulizwa kama amepokea maombi ya bodi ya kumtaka abadilishe uamuzi wake aligoma kuzungumzia kujiuzulu kwake na kusema atatoa tamko muda mwafaka ukifika. “Nimepokea simu nyingi kutoka kwa waandishi wa habari tangu asubuhi na jibu langu ni lilelile … sina cha kusema, tafadhali naomba respect (heshima)!” alisema Dk. Rashid ambaye alijiuzulu juzi jioni. Mwenyekiti wa Bodi ya Tanesco, Balozi Fulgence Kazaura alipoulizwa kama bodi hiyo ina mpango wa kumshawishi Dk. Rashid atengue uamuzi wake alisema: “Sina taarifa hiyo,” alisema. Kazaura alisema kuwa Dk. Rashid aliomba mwenyewe kujiuzulu juzi wakati wa Kikao cha Bodi bila kutoa sababu za hatua hiyo. “Hakusema kwa nini anajiuzulu lakini aliishukuru bodi kwa msaada iliyompa tangu aje kusaidia kuliboresha Shirika,” alisema Kazaura kwa sauti ya jazba na kumkatia simu mwandishi baada ya kumtaka aeleze sababu za mkurugenzi huyo kujiuzulu. Akizungumza na gazeti hili Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, alisema uamuzi wa mkurugenzi huyo hauwezi kuingiliwa na serikali kwa sababu yupo chini ya bodi lakini alikiri kupokea barua ya kujiuzulu kwa saa 24 kutoka kwa mkurugenzi huyo jana. “Ingekuwa amefukuzwa tungekuwa na maelezo ya kutoa lakini kwa sababu amejiuzulu mwenyewe maelezo yote yanapatikana kwa bodi lakini mimi nimepokea barua yake inayoeleza amejiuzulu,” alisema Waziri Karamagi ambaye hakuwa tayari kueleza zaidi. Naye Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu alisema serikali kwa sasa haiwezi kuzungumza lolote hasa kutokana na nafasi ya Rais kuwa mteuzi tu na kwamba kwa suala la kujiuzulu linaigusa moja kwa moja Bodi ya Tanesco ambayo ndiyo inayoripoti kazi kwake. “Mkurugenzi Mkuu wa Tanesco anaripoti kazi kwa bodi hivyo Rais yeye ni mteuzi tu wa anayeshika nafasi hiyo, hawezi kuingilia chochote. Nadhani bodi inahusika moja kwa moja na suala hili,” alisema Rweyemamu. Meneja Uhusiano wa Shirika hilo, Daniel Mshana alisema jana kuwa ni mapema kuzungumzia suala hilo na kuongeza kuwa kama kutakuwa na taarifa zozote kwa umma zitatolewa kwa wakati mwafaka. Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Tanesco, Stephen Mabada ambaye amekuwa anafanya kazi kwa karibu na Dk. Rashid alipoulizwa hali ikoje kwa wafanyakazi alisema ni ya kawaida na walikuwa wanaendelea kuchapa kazi kama kawaida. Licha ya mamlaka husika kutotaka kueleza sababu ya mkurugenzi huyo kujizulu, lakini baadhi ya vyanzo vya habari vimekuwa vinaeleza kuwa yeye ndiye aliyeshinikiza umeme kukatwa katika Kiwanda cha Saruji cha Tanga kutokana na kudaiwa Sh milion 49. Lakini bodi ilipingana na uamuzi wake ikieleza kuwa kiwanda hicho ni miongoni mwa wateja wakubwa lakini pia kinalipa kodi kubwa kwa serikali. Katika hali hiyo Dk. Idris akaona hawezi kufanya kazi katika mazingira ya ushauri wake kupingwa. Sababu nyingine inayotajwa kujiuzulu kwa mkurugenzi ni mpango wa shirika hilo kutaka kupandisha bei ya umeme kwa asilimia 40 na gharama za ufungaji kwa wateja wapya zaidi ya asilimia 150. Kuna madai kuwa bodi haikukubaliana na mpango huo kwa madai kuwa utawaumiza wananchi. Dk. Rashid aliteuliwa kushika wadhifa huo Novemba mwaka jana baada ya menejimenti ya Netgroup ya Afrika Kusini kumaliza muda wake Desemba 31 mwaka jana baada ya kuiongoza TANESCO kwa takriban miaka minne mfululizo kuanzia Mei, mwaka 2002. Wakati anatangaza uteuzi wake Balozi Kazaura alimwelezea Dk. Rashid, ambaye aliwahi kuwa Gavana wa Benki Kuu Tanzania (BoT) kati ya mwaka 1993 na 1998, kuwa mchumi kutokana na kuwa na Shahada ya Udaktari katika masuala ya Uchumi (PhD-Economics) aliyoipata katika Chuo Kikuu cha Boston, Massachusetts, nchini Marekani, Juni, 1984. ’’Uteuzi wa Dk. Rashid, umezingatia umuhimu wa kuwa na mtu mwenye uwezo mkubwa wa kusimamia masuala ya kifedha na pia ambaye ana uzoefu wa muda mrefu katika shughuli za menejimenti,’’ ilisema sehemu ya taarifa hiyo. Dk. Rashid pia aliwahi kuwa bosi NBC, Gavana wa BoT baada ya mkataba wake kumalizika hakutaka kuendelea badala yake akaenda kuongoza benki binafsi ya Akiba. Pia amewahi kuwa bosi wa Kampuni ya Simu ya Vodacom katika benki ya makabwela ya NMB na baadaye akateuliwa kuiongoza Tanesco wakati huo ikiwa taabani kifedha. Wachambuzi wa mambo waliotoa maoni yao kwa gazeti hili baadhi yao wamemsifu Dk. Rashid kwa kujiuzulu kwake kwani ameonyesha uadilifu wake kwa kuamua kuachia ngazi baada ya kuona mambo hayaendi ndani ya shirika hilo. Wengi wao wamekuwa wanaeleza kuwa huenda mtaalamu huyo wa mambo ya uchumi kaachia ngazi baada ya kuona kuna siasa katika uendeshaji wa shirika hilo. Wadau wengine wanafurahia kujiuzulu kwake kwa madai kuwa kama kweli ndiye aliyekuwa anang'ang'ania shirika hilo lipandishe gharama hizo hakuwa anajali wananchi walio wengi. "Huwezi kupandisha gharama ya umeme kwa asilimia 40 na huduma nyingine zaidi ya asilimia 100 bila kuwaonyesha watu kwanini unafanya hivyo." Dk. Rashid amejiuzulu wakati shirika hilo likiwa katika harakati za kupandisha gharama zake jambo ambalo linalalamikiwa na wananchi walio wengi. Leo wananchi wa Dar es Salaam watatoa maoni yao kuhusiana na mpango huo wa Tanesco. Wengine wanaeleza kuwa Tanesco inasema iko katika hali mbaya kwa sababu haikuwa ikikusanya madeni yake serikalini na katika mashirika ya umma na kwa kampuni binafsi, watumishi walikuwa wakiachia umeme huku wao wakikusanya fedha.

Copyright @TSN 2006 All Rights Reserved

COMEDY NI WAPI MNAPOJIMUVISHA ? UJUMBE GANI TUNAPEWA SASA TOILET AU GEST KUMBUKA WATOTO NDIO WENGI WANANGALIA ZE COMEDY P/SE WAPE KILICHO CHAO




Wednesday, November 21, 2007

Zitto Kabwe adai wanaopinga uteuzi wake wanatumiwa












Zitto Kabwe adai wanaopinga uteuzi wake wanatumiwa Zitto Kabwe adai wanaopinga uteuzi wake wanatumiwa
Wakati mgogoro kuhusu uteuzi wa mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe katika kamati ya madini ukiendelea kufukuta ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), mbunge huyo amesema baadhi ya watu wanaotoa kauli ya kupinga kuwako katika kamati ya kupitia upya mikataba ya madini wanatumiwa na makampuni ya madini bila kujua.
Akizungumza katika kipindi cha jana asubuhi cha Jambo Afrika kinachorushwa na Televisheni ya Taifa (TVT), Zitto alisema kuna baadhi ya watu wanatumiwa na makampuni ya uchimbaji madini bila kujua, kwani makampuni hayo hayataki kuchambuliwa kwa mikataba yao kwa sababu inawanufaisha wao zaidi kuliko Watanzania.
Nadhani baadhi yetu tunatumiwa na maadui zetu bila kujua, tunatumiwa na makampuni ya uchimbaji madini bila kujua, wao hawataki mikataba yao ichambuliwe kwani inawanufaisha wao zaidi kuliko sisi, alisema Zitto.
Alisema hoja ya kupitia upya mikataba ya madini ni Ilani ya Chadema na yeye ndiye aliwasilisha bungeni sasa ikiwa Rais kaamua kuunda kamati katumia ilani ya chama chao kuna kosa gani yeye kuwemo.
Zitto pia aliwapinga wanaosema hamati hiyo haina nguvu kisheria kwa kuwa haikuteuliwa na Bunge, kwa maelezo kwamba hoja zao hazina nguvu.
Alisema kimsingi, Rais ni mkuu wa nchi hivyo ana uwezo kumwita mtu yeyote na hata kamati aliyounda ina mamlaka hayo.
Hoja kwamba kamati iliyoundwa na rais kupitia mikataba ya madini haina nguvu kisheria haina nguvu, kwani yeye ndie Amiri Jeshi Mkuu na kamati hiyo ina uwezo na uhuru wa kumuita yoyote na kumhoji ili kupata ushahidi, alisema Zitto.
Alisema sio mara ya kwanza kuteuliwa katika kamati ya rais na sasa anashangaa ni kwanini uteuzi wa hivi karibuni umezua mjadala mkubwa. Zitto amewahi kuteuliwa katika Kamati ya kukusanya maoni ya uundwaji Shirikisho la Afrika Mashariki.
Hata hivyo, alisema kuwa anasubiri Kamati Kuu ya chama chake ikae Jumaamosi ijayo na kutoa kauli ambayo ataiheshimu. Maamuzi ya Kamati Kuu ndio maamuzi yangu, ikisema nitoke nitatoka, alimalizia Zitto.
Awali katika majadikliano hayo Mbunge wa Tarime (Chadema) Chacha Wangwe ambaye amekuwa akipinga uteuzi wa Zitto alisema kamati hiyo haina nguvu kisheria kwani hoja ya kuundwa kwake ilitoka katika mkutano wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na sio bungeni kama wapinzania walivyokuwa wanataka.
Alisema Kamati haiwezi hata kutangaza matokeo yatakayopatikana bali itapeleka ripoti kwa rais.
Katika hatua nyingine, ratiba ya ziara ya kamati ya kuangalia upya mikataba ya uchimbaji wa madini nchini katika nchi mbalimbali duniani, itatangazwa rasmi wiki ijayo.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Jaji Mark Bomani aliliambia Mwananchi jijini Dar es Salaam jana kuwa wanatarajia kutangaza ratiba hiyo Jumanne wiki ijayo, lakini hakuwa tayari kueleza nchi anayokwenda.
Wakati huo huo; Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, anawasili nchini leo kuongoza Kikao Cha Kamati Kuu ya chama hicho (CC) itakayojadili uteuzi wa Mbunge wake Zitto Kabwe katika Kamati ya Madini.
Pia Kamati ya Ufundi ya Muungano wa Vyama vya Upinzani imekutana kuzungumzia suala hilo.
Kamati hiyo ambayo iko chini ya mwenyekiti, Benedict Mutungilei wa TLP, imekutana na kujadili suala la mbunge huyo kuwapo katika Kamati hiyo na kutoa mapendekezo yake kwa wenyeviti wa vyama vilivyo katika muungano huo.
Wajumbe wengine wa Kamati hiyo iliyokutana juzi na jana ni Hussein Mmasi kutoka Chama cha Wananchi (CUF), Sam Luhuza na Ndelakia Kessy wa NCCR-Mageuzi, Erasto Tumbo na John Mrema kutoka Chadema.

Richa yupo na Tekonolojia hipo kazi kwako


QUEEN ELIZABETH NDANI YA UGANDA

Queen Elizabeth



Queen Elizabeth arrives in Uganda

KAMPALA: Britain's Queen Elizabeth II arrived in Uganda Wednesday ahead of the Commonwealth Heads of Government meeting, on her first visit to the country in more than half a century. The monarch and her husband Prince Philip, the Duke of Edinburgh, landed at the newly-upgraded Entebbe airport, on the shores of Lake Victoria, amid tight security and media restrictions. The 81-year-old queen was last in Uganda in 1954, long before the East African country -- hosting the Commonwealth's biennial summit for the first time -- acquired its independence from Britain. She was in Kenya when she acceded to the throne in 1952, upon the death of her father King George VI. Uganda has long felt overshadowed by its neighbour Kenya, considered the African jewel of the former British empire. Officials are hoping that the meeting of former colonies -- the largest event ever hosted by Uganda -- will raise the country's profile in the region and help kickstart tourism. Also attending the Commonwealth summit will be the heir to the British throne Prince Charles and his wife Camilla, the Duchess of Cornwall. It will be Charles's first attendance at a Commonwealth summit, amid speculation that the 53-state organisation is preparing for life after Elizabeth.

Vyama vya upinzani CUF, TLP vyajadili kuhusu Zitto





















Vyama vya upinzani CUF, TLP vyajadili kuhusu Zitto

*Wawaasa Chadema wazungumzie hoja ya msingi

* Wasema mjadala ulenge katika rasilimali za nchi

*Makani ataka Zitto aingie jikoni kupakua ukweli

Na Waandishi Wetu


VYAMA vya CUF na TLP, vimewataka viongozi wa Chadema kuacha kujadili uteuzi wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe katika kamati ya kuangalia upya mikataba ya uchimbaji madini nchini na badala yake kisisitize mjadala katika hoja ya msingi.
CUF na TLP, vimesema wanachopaswa Chadema na jamii kwa jumla hivi sasa ni kukijadili kuhusiana na suala zima la ufisadi katika rasilimali za nchi, badala ya kumjadili Zitto.
Akizungumza na Mwananchi ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa TLP Taifa Augustine Mrema, alisema kuwa Chadema na jamii hawapaswi kumzungumzia Zitto, badala yake wanachotakiwa kukifanya ni kuzungumzia hoja ya msingi na kutokubali kutolewa nje ya hoja hiyo.
�Ikiwa jamii na viongozi wa Chadema watakubali kutolewa nje ya hoja ya msingi ya ufisadi na kuingizwa katika kumjadili Zitto watakuwa wamekosea,� alisema Mrema.
Alisema uteuzi wa Zitto katika kamati hiyo sio suala la kujadili kwani angeweza kuchaguliwa yeyote, bali linalopaswa kujadiliwa ni dhamira ya Rais Jakaya Kikwete ya kuunda kamati hiyo.
Naye Kaimu Mkurugenzi wa Haki za Bindamu na Mahusiano na Umma wa CUF, Mbaralah Maharagande, alisema maoni tofauti yanayotolewa na viongozi wa Chadema kuhusiana na uteuzi wa Zitto kwenye kamati hiyo, ni ya mtu mmoja mmoja na sio kauli ya pamoja.
Alisema kinachopaswa kujadiliwa hivi sasa, ni kuhusu ufisadi katika matumizi ya rasilimali za nchi, mikataba yenye utata ya uchimbaji wa madini, ikiwa ni sehemu moja tu ya ufisadi huo hapa nchini.
�Suala sio kujadili uteuzi wa Zitto katika kamati ya madini, tusikubali kuchezewa hisia zetu kwa kutolewa nje ya hoja kuu, suala ni kwamba kamati haiwezi kutoa matunda yaliyokusudiwa�, alisema Maharagande.
Hata hivyo, Maharagande alisema ushirikiano wa vyama vya upinzani, wanatarajia kufanya mkutano wa pamoja ambapo kupitia mkutano huo watatoa tamko la pamoja juu ya kamati ya madini na uteuzi wa Zitto katika kamati hiyo.
Hata hivyo, wakati viongozi wa CUF na TLP wakisema hayo, Makani ambaye pia ni mmoja wa waasisi wa Chadema alisema jana kuwa anaunga mkono uteuzi wa Zitto, lakini akasema ana wasiwasi na baadhi ya watu kuwamo katika kamati hiyo kwa kuwa walishiriki katika kuandika mikataba ya madini.
Aliwataja wanakamati hao kuwa ni pamoja na mjumbe kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na mwingine kutoka Wizara ya Nishati na Madini ambao alisema walipaswa kuwa mashahidi zaidi kuliko kuwa wanakamati.
"Kuna uwezekano wa watu hao kuitetea mikataba waliyoshiriki kuitayarisha," alisema Makani.
Hata hivyo, alisema dosari hiyo haiwezi kuwa ya msingi kiasi cha kuamua kuisusa kamati nzima kutokana na umuhimu wa madini hapa nchini.
Alisema suala la madini ambayo ni miongoni mwa rasilimali za nchi, si jambo la siasa au itikadi na kwamba, Ilani ya Chadema ilikwishaeleza mapema kwamba, mikataba ya uchimbaji madini ina matatizo na kwa sababu hiyo, ndiyo iliyomfanya Zitto aipeleke hoja hiyo bungeni kwa kuwa alikuwa anatekeleza Ilani ya chama chake.
"Alitimiza wajibu wake kama mbunge," alisema Makani.
Kutokana na hali hiyo, alisema anaunga mkono uteuzi wa mbunge huyo kwenye kamati hiyo kwa asilimia mia moja kwa kuwa utamwezesha kuwa karibu zaidi, kupambanua na kubainisha ukweli juu ya yote yatakayoshughulikiwa na kamati hiyo.
"Kufuatana na hayo, sina tatizo la uteuzi wa Zitto kwenye kamati hiyo, sina tatizo kabisa. Zitto aingie jikoni na kupakua kwa sababu anatetea maslahi ya nchi," alisema Makani na kuongeza:
"(Zitto) Akiona wanakamati wanakwenda kinyume na msimamo ambao hauna maslahi ya nchi, atakuwa huru kuandika ripoti ya kutofautiana na ripoti itakayokuwa imeandikwa na kamati.
Wengine ambao wameshatamka wazi kwamba wanamuunga mkono, Zitto kuwako katika kamati hiyo ni pamoja na mwasisi wa Chadema, Edwin Mtei. Pia Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amenukuliwa na vyombo vya habari vya nje, akisema yeye binafsi haoni tatizo kwa Zitto kuwako katika kamati hiyo.
Tayari Mbowe, ameitisha kikao cha Kamati Kuu ambacho kinatarajiwa kufanyika Jumamosi kujadili pamoja na mambo mengine uteuzi wa Zitto katika kamati ya kupitia upya madini.
Novemba 13, Mwaka huu, Rais Kikwete alitangaza kuundwa kwa Kamati ya kupitia mikataba na sheria za madini na kuwateua wajumbe wa kamati hiyo iliyojumuisha wajumbe kutoka kambi ya upinzani akiwemo Zitto wa Chadema na Mwenyekiti wa United Democratic Party (UDP) ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi Mashariki, John Cheyo.
Tangu Rais Kikwete aunde kamati hiyo na kumteua Zitto kuwa mmoja wa wajumbe wake (kamati hiyo), baadhi ya watu, wakiwamo wafuasi wa chama hicho wakiongozwa na Mbunge wa Tarime (Chadema), Chacha Wangwe, wameripotiwa na vyombo vya mawasiliano na jamii wakipinga uteuzi huo wa Zitto kwa madai kwamba, unadhoofisha hoja za wapinzani na kujenga usaliti baina yao kuhusiana na suala la madini nchini.
Kamati hiyo yenye wajumbe 12, iko chini ya uenyekiti wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mstaafu, Jaji Mark Bomani.
Wengine wanaounda kamati hiyo, ni Mwanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini, Salome Makange, Kamishina wa Sera Wizara ya Fedha, Mugisha Kamugisha, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Makazi Wizara ya Ardhi, Edward Kihundwa na Mbunge wa Kyela (CCM), Dk Harrison Mwakyembe.
Wajumbe wengine, ni Mbunge wa Msalala (CCM), Ezekiel Maige, Peter Machunde kutoka Soko la Hisa, Dar es Salaam (DSE), Mkaguzi wa Mahesabu kutoka Kampuni ya Kimataifa ya Ukaguzi wa Mahesabu, PriceWaterHouseCoopers, David Tarimo ambaye ni mtaalamu wa masuala ya kodi na Mkurugenzi wa Madai na Sheria za Kimataifa, Wizara ya Katiba na Sheria, Maria Kejo.





Imeandaliwa na Muhibu Said, Elizabeth Suleyman, Salim Said na Mwanaid Omary wa MUM.


Aliyepasuliwa kichwa kwa makosa MOI sasa alishwa kwa mrija

Na Mwandishi Wetu


MGONJWA Emmanuel Didas aliyepasuliwa kichwa badala ya mguu Novemba mosi mwaka huu katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) ameanza kulishwa chakula kwa kutumia mpira baada ya kushindwa kula kwa njia ya kawaida.
Hali ya mgonjwa huyo imezidi kuwa mbaya baada ya kupooza upande wa kulia na hivi sasa hawezi kula kwa njia ya kawaida badala yake anatumia mrija tangu jana usiku tofauti na alivyokuwa alipotolewa katika Chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU).
Wakizungumza na Mwandishi wa habari hizi jana hospitalini hapo huku wakiomba majina yao yasitajwe gazetini kwa lengo la kulinda ajira zao baadhi ya watumishi wa hospitali hiyo walithibitisha kuwa mgonjwa huyo anakula kwa kutumia mpira .
�Awali tulikuwa tunamlisha kwa njia ya kawaida, lakini tangu jana tunamlisha kwa njia ya mpira hali hii inazidi kumdhoofisha kwasababu chakula anachokula kwa njia ya mpira si kingi ukilinganisha na alichokuwa anakula kwa njia ya kawaida,� alisema mmoja watumishi hao.
Ndugu wa mgonjwa aliyefika wodini hapo kwa ajili ya kumpelekea chakula alifahamisha kuwa mgonjwa huyo analishwa na wauguzi kwa njia ya mpira na kwamba hali yake imezidi kudhoofu.
Mwandishi wa habari hizi alimtafuta kaka wa mgonjwa huyo ambaye ndiye msemaji wa familia hiyo, Sists Marishay ambaye alisema kwamba hajafika hospitalini hapo tangu asubuhi hivyo hakufahamu maendeleo yake kwa leo.
�Tangu asubuhi (jana) sijaenda kumuona kwa hiyo sifahamu maendeleo yake nitakapofika huko nitakupa taarifa kamili,� alisema Marishay.
Mgonjwa mwenzake Emmanuel Mgaya aliyefanyiwa upasuaji wa kichwa badala ya mguu juzi alifanyiwa upasuaji wa kichwa ili kuondoa tatizo ambalo lilikuwa linamsumbua hali yake pia imeelezwa kuwa dhaifu tofauti na jana muda mfupi baada ya kufanyiwa upasuaji huo na amelazwa ICU akiendelea kuhudumiwa kwa karibu na madaktari wa taasisi hiyo.
Baadhi ya madaktari wanaomuhudumia walisema mabadiliko yake yanaoneka kutokana na anavyopumua kwasababu kwa sasa anapumua kwa shida tofauti na alivyo kuwa juzi baada ya kufanyiwa upasuaji huo.
Hata hivyo wasemaji wa hospitali hiyo walipotafutwa ili wazungumzie hali ya wagonjwa hao waliwakimbia waandishi kwa visingizio mbalimbali.
Afisa Uhusiano wa Taasisi hiyo, Jumaa Almasi alionekana na alipoulizwa alidai kwamba anakwenda kutafiti hali za wagonjwa hao na hakurudi tena na msaidizi wake Mary Ochieg alisemakuwa yeye si msemaji wa taasisi hiyo kisha akafunga mlango wa Ofisi yake na kuondoka.
Naye Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Profesa Laurent Museru alipotafutwa ana kwa ana hakupatikana na alipopigiwa simu ili azungumzie hali ya wagonjwa hao alikata simu na kuzima kabisa baada ya kugundua kuwa anazungumza na mwandishi wa habari.
Wagonjwa hao walifanyiwa upasuaji tofauti na matatizo yao Novemba mosi, mwaka huu katika taasisi hiyo na kutokana na utata uliojitokea baada ya makosa hayo kufanyika, Mkurugenzi wa Taasisi hiyo aliunda tume ya kuchunguza tukio hilo ambayo ilikamilisha kazi yake na kukabidhi ripoti yao kwa Bodi ya wadhamnini wa MOI Novemba 16, mwaka huu na Novemba 16 ikapelekwa kwa Waziri wa Afya na Ustawi ya Jamii, Profesa Devid Mwakyusa kwa hatua zaidi
.

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.comme google-site-verification=Qm-XNfnL5kai8WV2inT1RRX2WIPaBTG_WPq3kYSBwbgKennedy Kimaro 2008 NYUMBANI NI NYUMBANI TU KUMBUKA KUWEKEZA NYUMBANI LEO

Rudi TOP-Juu