Sunday, April 13, 2008

Harusi yageuka msiba

HABARI Harusi yageuka msiba ::: 50 Cent kuzuru nchini Mei ::: Maathai ajitoa kukimbiza mwenge ::: Stars kufuta machungu ya Watanzania? ::: NICOL yajinadi Singida ::: Wavuvi wataka bei rasmi ya samaki ::: Nokia kufungua tawi Tanzania ::: Zantel yazindua huduma ya kibenki ::: TSN yazindua ofisi Mbeya ::: Wizara yaweka kipaumbele ushirikishwaji wanawake ::: Mchakato kuanzisha Baraza la Vijana waingia dosari ::: Mfanyabiashara maarufu Mererani auawa kwa risasi ::: Wizara, Idara, Wakala za serikali zafuja bilioni 25/- ::: Maandamano makubwa ya CUF Zanzibar ::: Rostam apigwa stop ::: Kampuni zisiishie kuleta wasanii wa nje tu ::: Bila klabu bora timu ya Taifa bora ni njozi ::: TMK wanaume Halisi, Family kumaliza ubishi leo ::: Ally aibuka bingwa wa Fiddle ::: Milioni 21 kukarabati Uwanja wa Umoja ::: AFC yabanwa ligi ya mkoa ::: Karate U-17 kuwasha moto Dar ::: Nokia yajiimarisha kupata wateja wa kipato cha chini ::: Wazuiwa kuchuuza pembeni mwa barabara ::: Barrick waagizwa kujenga uzio mgodini ::: Wateja wapya Stanchart kuzawadiwa ::: Atoa ushuhuda wa mauaji ya Rwanda ::: Malipo kwa waliobomolewa Tabata Dampo yaidhinishwa ::: Mjadala kubadili mitaala kidato cha tano waanza ::: Wabunge waunga mkono ukodishaji wa rasilimali :::

Jumapili Apr 13, 2008
Umati wa watu waliohudhuria maandamano na mkutano wa CUF mjini Zanzibar jana.
HABARI INAYOONGOZA LEO::

Harusi yageuka msiba
WATU wanane, akiwamo bi harusi mtarajiwa aliyekuwa akisafiri kuhudhuria Kitchen party, wamekufa katika ajali ya barabarani iliyohusisha magari matatu, likiwamo basi lililokuwa limebeba maiti.

Watu saba kati ya hao walikufa papo hapo baada ya basi la Meridian kuligonga kwa nyuma basi dogo la Toyota Hiace lililokuwa limembeba bibi harusi mtarajiwa, mama yake mzazi, nduguze, mpambe wake na jamaa waliokuwa wakisafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Tanga, juzi jioni.

Polisi wamemtaja msichana huyo kuwa ni Irene Stephen Hizza (22) aliyekuwa mkazi wa Mbezi Beach, Dar es Salaam aliyekuwa akisoma katika Chuo Cha Elimu ya Biashara (CBE) jijini. Mpambe wake pia alikufa katika ajali hiyo.

Jana alasiri bwana harusi mtarajiwa, Ramadhani Lukuta alilieleza HabariLeo Jumapili kuwa Irene na wenzake walikuwa wakienda Tanga kwa ajili ya sherehe za kumuandaa bibi harusi, maarufu kama Kitchen party.

Kwa mujibu wa mkazi huyo wa Dar es Salaam, aliyekuwa mkewe mtarajiwa anatarajiwa kuzikwa leo katika Kijiji cha Lusanga wilayani Muheza mkoani Tanga na kwamba miili mingine mitatu ingesafirishwa jana jioni kuletwa Dar es Salaam.

Ilikuwa imepangwa kwamba harusi baina ya Irene na Lukuta ingefanyika Aprili 26. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Simoni Sirro alisema jana kuwa basi la Meridian liliigonga Hiace hiyo juzi saa moja usiku katika Kijiji cha Kitumbi wilayani Handeni.

Aliwataja marehemu wengine kuwa ni mpambe wa bibi harusi, Latifa Undole (23) aliyekuwa akisoma CBE Dar es Salaam, Dafroza Mapunda (23) aliyekuwa akisoma katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Dar es Salaam, na George Hizza (11) aliyekuwa akisoma darasa la sita katika Shule ya Mtakatifu Maria, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Polisi, marehemu wengine ni Neema Chedi (26) mkazi wa Dar es Salaam aliyekuwa akifanya kazi Mamlaka ya Bandari, dereva wa Hiace, Zuberi Mohammed (35), mama Masatu (45) na mwingine aliyetambuliwa kwa jina moja la Mariam aliyekuwa akiishi Dar es Salaam.

Kamanda Sirro alisema watu 12 walijeruhiwa katika ajali hiyo, watatu wamelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na tisa wamelazwa katika Hospitali ya Korogwe. Kwa mujibu wa Kamanda Sirro, basi la Meridian lililokuwa likiendeshwa na Edward Temu (35) lilikuwa limebeba maiti aliyekuwa akisafirishwa kutoka Dar es Salaam kwenda Moshi mkoani Kilimanjaro.

Kamanda Sirro alisema, kabla ya ajali hiyo, Hiace hiyo ilikuwa mbele ya basi la Meridian yote yakiwa katika mwelekeo mmoja na kulikuwa na lori mbele yao. Alisema, wakati yakiendelea na safari, dereva wa Hiace alipunguza mwendo kuepuka kugongana uso kwa uso na basi la Scandnavia aina ya Isuzu Nissan lililokuwa kwenye mwendo mkali.

Sirro alisema baada ya basi hilo dogo kupunguza mwendo, basi la Meridian lililokuwa kwenye mwendo mkali liligonga kwa nyuma na kusababisha Hiace hiyo iligonge lori aina ya Fuso na gari hilo dogo likapinduka.

Kwa mujibu wa Mwandishi Wetu wa Tanga, waliojeruhiwa katika ajali hiyo ni Anna Alli (48), Anase Meridiani (30), Sophia Vicent (22), Aisha Rashid (29), Barnabas Vallerian (44), Anna Mhina (48), Nora Msindai (22), Sekuza Nyamwanga (30) na Laurance Ndiu (30), wote wakazi wa Dar es Salaam. Wengine ni Doris Mhina mkazi wa Tanga na Samweli Shirima (22) mkazi wa Rombo mkoani Kilimanjaro.


WATU wanane, akiwamo bi harusi mtarajiwa aliyekuwa akisafiri kuhudhuria Kitchen party, wamekufa katika ajali ya barabarani iliyohusisha magari matatu, likiwamo basi lililokuwa limebeba maiti.

Watu saba kati ya hao walikufa papo hapo baada ya basi la Meridian kuligonga kwa nyuma basi dogo la Toyota Hiace lililokuwa limembeba bibi harusi mtarajiwa, mama yake mzazi, nduguze, mpambe wake na jamaa waliokuwa wakisafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Tanga, juzi jioni.

Polisi wamemtaja msichana huyo kuwa ni Irene Stephen Hizza (22) aliyekuwa mkazi wa Mbezi Beach, Dar es Salaam aliyekuwa akisoma katika Chuo Cha Elimu ya Biashara (CBE) jijini. Mpambe wake pia alikufa katika ajali hiyo.

Jana alasiri bwana harusi mtarajiwa, Ramadhani Lukuta alilieleza HabariLeo Jumapili kuwa Irene na wenzake walikuwa wakienda Tanga kwa ajili ya sherehe za kumuandaa bibi harusi, maarufu kama Kitchen party.

Kwa mujibu wa mkazi huyo wa Dar es Salaam, aliyekuwa mkewe mtarajiwa anatarajiwa kuzikwa leo katika Kijiji cha Lusanga wilayani Muheza mkoani Tanga na kwamba miili mingine mitatu ingesafirishwa jana jioni kuletwa Dar es Salaam.

Ilikuwa imepangwa kwamba harusi baina ya Irene na Lukuta ingefanyika Aprili 26. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Simoni Sirro alisema jana kuwa basi la Meridian liliigonga Hiace hiyo juzi saa moja usiku katika Kijiji cha Kitumbi wilayani Handeni.

Aliwataja marehemu wengine kuwa ni mpambe wa bibi harusi, Latifa Undole (23) aliyekuwa akisoma CBE Dar es Salaam, Dafroza Mapunda (23) aliyekuwa akisoma katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Dar es Salaam, na George Hizza (11) aliyekuwa akisoma darasa la sita katika Shule ya Mtakatifu Maria, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Polisi, marehemu wengine ni Neema Chedi (26) mkazi wa Dar es Salaam aliyekuwa akifanya kazi Mamlaka ya Bandari, dereva wa Hiace, Zuberi Mohammed (35), mama Masatu (45) na mwingine aliyetambuliwa kwa jina moja la Mariam aliyekuwa akiishi Dar es Salaam.

Kamanda Sirro alisema watu 12 walijeruhiwa katika ajali hiyo, watatu wamelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na tisa wamelazwa katika Hospitali ya Korogwe. Kwa mujibu wa Kamanda Sirro, basi la Meridian lililokuwa likiendeshwa na Edward Temu (35) lilikuwa limebeba maiti aliyekuwa akisafirishwa kutoka Dar es Salaam kwenda Moshi mkoani Kilimanjaro.

Kamanda Sirro alisema, kabla ya ajali hiyo, Hiace hiyo ilikuwa mbele ya basi la Meridian yote yakiwa katika mwelekeo mmoja na kulikuwa na lori mbele yao. Alisema, wakati yakiendelea na safari, dereva wa Hiace alipunguza mwendo kuepuka kugongana uso kwa uso na basi la Scandnavia aina ya Isuzu Nissan lililokuwa kwenye mwendo mkali.

Sirro alisema baada ya basi hilo dogo kupunguza mwendo, basi la Meridian lililokuwa kwenye mwendo mkali liligonga kwa nyuma na kusababisha Hiace hiyo iligonge lori aina ya Fuso na gari hilo dogo likapinduka.

Kwa mujibu wa Mwandishi Wetu wa Tanga, waliojeruhiwa katika ajali hiyo ni Anna Alli (48), Anase Meridiani (30), Sophia Vicent (22), Aisha Rashid (29), Barnabas Vallerian (44), Anna Mhina (48), Nora Msindai (22), Sekuza Nyamwanga (30) na Laurance Ndiu (30), wote wakazi wa Dar es Salaam. Wengine ni Doris Mhina mkazi wa Tanga na Samweli Shirima (22) mkazi wa Rombo mkoani Kilimanjaro.

  © Blogger templates 'Neuronic' by Ourblogtemplates.comme google-site-verification=Qm-XNfnL5kai8WV2inT1RRX2WIPaBTG_WPq3kYSBwbgKennedy Kimaro 2008 NYUMBANI NI NYUMBANI TU KUMBUKA KUWEKEZA NYUMBANI LEO

Rudi TOP-Juu